• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
Lita 4,500 za Dizeli ya soko la nje zanaswa Kisumu

Lita 4,500 za Dizeli ya soko la nje zanaswa Kisumu

Na BERNARDINE MUTANU

TUME ya Kudhibiti Mafuta nchini (ERC) Ijumaa imetoa taarifa kuhusu operesheni kumaliza biashara haramu ya mafuta eneo la Otonglo, Kaunti ya Kisumu.

Operesheni hiyo ilifanywa Jumatano na maafisa wa uchunguzi wa kihalifu (DCI) na police wa  GSU ambao walipata lita 4,500 za dizeli ya kuuza nje.

Wakati wa operesheni hiyo, washukiwa watano walikamatwa na gari lenye nambari ya usajili KAN 022 C. Watano hao walifikishwa mahakamani Jumatano na kushtakiwa kwa kuendesha biashara bila leseni kinyume cha sheria.

Kituo hicho pia kiliharibiwa kwa mujibu wa sheria, ilisema ERC.

You can share this post!

Wakana mashtaka 151 ya kughushi hati za ajali kudai fidia

Hamtatuweza, Ruto na Waiguru wafokea wakosoaji

adminleo