• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 7:50 AM
Apple yazindua simu ghali zaidi, iPhone XS Max

Apple yazindua simu ghali zaidi, iPhone XS Max

MASHIRIKA Na PETER MBURU

Los Angeles, AMERIKA

KAMPUNI ya kutengeneza simu Apple imezindua simu mpya ambayo inagharimu zaidi ya Sh100,000, ikiwa ndiyo ya bei ghali zaidi kuwahi kuzinduliwa hadi sasa.

Katika hafla iliyoandaliwa eneo la Cupertino, California Marekani Jumatano kampuni hiyo ilizindua simu tatu aina ya smartphone iPhone XS, iPhone XS Max na iPhone XR ambazo ni za muundo wa hali ya juu.

Kampuni hiyo ya US sasa itauza simu ya XS Max kwa Sh109,900 ikiwa ndiyo simu ghali zaidi ambayo kampuni ya Apple imewahi kutengeneza. Ukubwa kioo chake ni inchi 6.5.

Nayo simu aina ya iPhone XS ina ukubwa wa kioo wa inchi 5.8 na itauzwa kwa Sh99,900, huku ya iPhone XR ikiuzwa Sh74,900 na ikiwa na ukubwa wa kioo wa inchi6.1. Rangi za simu hizo ni bluu, manjano na nyekundu.

Simu hizo mbili za iPhone XS na iPhone XS Max zitakuwa za kwanza kuwa na uwezo wa kutumia kadi mbili za simu (dual sim).

Nambari moja ya simu itahifadhiwa kwenye simukadi ya kielektroniki, kasha mtumizi kuongeza simukadi nyingine.

Muundo wa iPhone ndiyo mali kubwa zaidi ya kampuni ya Apple na ambao umeipa mapato ya zaidi ya thuluthi mbili.

You can share this post!

Zimbabwe yapiga marufuku mikutano ya umma Chamisa akipanga...

Dume ‘lililosafiri mbinguni’ lasema linapanda...

adminleo