• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Simbas kuraruana na Romania na Namibia kabla ya mchujo wa Kombe la Dunia

Simbas kuraruana na Romania na Namibia kabla ya mchujo wa Kombe la Dunia

Na Geoffrey Anene

KENYA Simbas itasakata mechi nne za kujipima nguvu kati ya Oktoba 7 na Novemba 3 kabla ya mchujo wa kufa-kupona wa kufuzu kushiriki Kombe la Dunia la raga ya wachezaji 15 kila upande nchini Ufaransa hapo Novemba 11-23, 2018.

Simbas ilikuwa imeomba Shirikisho la Raga la Kenya (KRU) kuitafutia mechi mbili za kirafiki, lakini taarifa kutoka shirikisho hilo zinasema kwamba vijana wa kocha Ian Snook watalimana na British Army kutoka Nanyuki, mabingwa wa Afrika Namibia, klabu ya Blue Bulls kutoka Afrika Kusini na timu ya taifa ya Romania kabla ya kuelekea mjini Marseille.

Kenya inafahamu British Army kwa sababu imefanya mazoezi mara kadhaa nayo katika milima ya Nanyuki. Ilijitayarisha kwa mechi yake ya mwisho ya Kombe la Afrika la Dhahabu dhidi ya Namibia kwa kufanya mazoezi na British Army, ingawa ilipoteza 53-28 jijini Windhoek na kuingia mchujo huu wa mwisho, huku Namibia ikijikatia tiketi ya kuelekea Japan mwaka 2019 kama bingwa wa wa Afrika.

Simbas inajua Namibia kutokana na mashindano ya kila mwaka ya Kombe la Afrika, lakini haijawahi kukutana na Blue Bulls wala Romania.

Simbas itamenyana na Canada, Hong Kong na Ujerumani katika mchujo wa kuingia Kombe la Dunia. Mshindi wa mchujo huu wa mataifa manne atajaza nafasi ya 24 (mwisho) iliyosalia. Atatiwa katika Kundi B pamoja na New Zealand, Afrika Kusini, Italia na Namibia.

Ratiba na matokeo ya Simbas mwaka 2018:

Oktoba 7

Kenya na British Army (Kirafiki, Nairobi)

Oktoba 21

Kenya na Namibia (Kirafiki, Nairobi)

Oktoba 28

Kenya na Blue Bulls kutoka Afrika Kusini (Kirafiki, Nairobi)

Novemba 3

Romania A na Kenya (Kirafiki, Bucharest)

Novemba 11

Canada na Kenya (Mechi ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia, 6.30pm Marseille, Ufaransa)

Novemba 17

Hong Kong na Kenya (Mechi ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia, 4.00pm Marseille, Ufaransa)

Novemba 23

Kenya na Ujerumani (Mechi ya kufuzu kushiriki Kombe la Dunia, 8.00pm Marseille, Ufaransa)

Juni 23

Morocco 24-28 Kenya

Juni 30

Kenya 45-36 Zimbabwe

Julai 7

Kenya 38-22 Uganda

Agosti 11

Kenya 67-0 Tunisia

Agosti 18

Namibia 53-28 Kenya

You can share this post!

Apigwa marufuku mechi 27 kwa kukwaruza kichuna wake kifuani

Mtu na mkewe kizimbani kwa wizi wa shamba la mamilioni

adminleo