• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Simanzi katika hafla ya waliokufa katika ajali ya ndege

Simanzi katika hafla ya waliokufa katika ajali ya ndege

Hafla ya mazishi ya watu wawili walioangamia katika ajali ya ndege Oktoba 21, 2017, yafanyika katika ufuo wa Ziwa Nakuru Februari 10, 2018. Picha/ Joseph Openda

Na PETER MBURU

Kwa muhtasari:

  • Mazishi hayakuwa na jeneza, bali maua na picha pekee
  • Sam G na Mapozi hawakuwahi kupatikana tangu ajali ya Nakuru itokee
  • Babake Mapozi naye alieleza huzuni yake, akisema mwanawe alikuwa amependekeza mahali alipotaka kujenga nyumba ya kifahari
Hafla ya mazishi ya watu wawili walioangamia katika ajali ya ndege Oktoba 21, 2017, yafanyika katika ufuo wa Ziwa Nakuru Februari 10, 2018. Picha/ Joseph Openda

MAJONZI yalitanda Jumamosi katika ufuo wa Ziwa Nakuru wakati wa sherehe ya mazishi ya ukumbusho wa pamoja kwa watu wawili kati ya watano walioangamia kwenye ajali ya ndege mwaka 2017.

Kinyume na mazishi ya kawaida ambapo kungekuwa na majeneza, ni picha zao nadhifu pamoja na maua vilivyowekwa mezani katika hema.

Wawili hao, Samuel Gitau (Sam G) na John Ndirangu Njuguna (Mapozi) waliangamia pamoja na wenzao watatu Anthony Kipyegon, rubani Apollo Malowa na mwanadada Veronica Muthoni.

Hafla ya mazishi ya watu wawili walioangamia katika ajali ya ndege Oktoba 21, 2017, yafanyika katika ufuo wa Ziwa Nakuru Februari 10, 2018. Picha/ Joseph Openda

Japo watatu hao walipatikana na maiti zao kuzikwa nyumbani mwao, Sam G na Mapozi hawakuwahi kupatikana, jambo lililosukumia viongozi, familia na marafiki kupendekeza sherehe ya aina hiyo, kama njia mojawapo ya kuliwaza familia zao.

Jumamosi wakati wa maombelezi hayo, viongozi wa tabaka mbalimbali waliungana na familia za wendazao katika ufuo huo tangu ajali hiyo mwezi Oktoba.

Picha za ‘Mapozi’ na ‘Sam G’ walioangamia katika ajali ya ndege Oktoba 21, 2017. Mazishi yao yalifanyika katika ufuo wa Ziwa Nakuru Februari 10, 2018. Picha/ Joseph Openda

“Tumepitia miezi mitatu na nusu ya kuchosha, kutamausha na kuvunja moyo tulipokuwa tukitafuta miili ya wapendwa wetu,” seneta wa Nakuru Susan Kihika, ambaye pia alikuwa mwajiri wao akasema.

Babake ‘Mapozi’ naye alieleza huzuni yake, akisema mwanawe alikuwa amependekeza mahali alipotaka kujenga nyumba ya kifahari, lakini akafa kabla ya kutimiza ndoto yake.

 

You can share this post!

Makanisa yataka serikali izime ‘Samantha’

Msomi ataka ushirikiano Pwani

adminleo