• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 5:22 PM
Romania yataja kikosi kitakachovaana na Simbas Bucharest

Romania yataja kikosi kitakachovaana na Simbas Bucharest

Na GEOFFREY ANENE

NCHI ya Romania imetaja kikosi chake kitakachopimana nguvu na Kenya Simbas katika mechi ya raga ya wachezaji 15 kila upande jijini Bucharest hapo Novemba 3, 2018.

Romania haijawahi kukutana na Kenya katika mechi ya raga. Simbas ya kocha Ian Snook iliondoka jijini Nairobi mnamo Oktoba 31 ikipitia Ufaransa. Italimana na Romania kuanzia saa nane mchana Jumamosi.

Mabingwa wa Afrika mwaka 2011 na 2013 Kenya wanatumia mchuano huu, ambao utapeperushwa na runinga ya Romania ya Telekom Sport, kujiandaa kwa mchujo wa mwisho wa kuingia Kombe la Dunia mwaka 2019.

Mchujo wenyewe utafanyika mjini Marseille nchini Ufaransa kati ya Novemba 11 na Novemba 23 ukikutanisha Kenya, Canada, Hong Kong na Ujerumani. Mshindi atajikatia tiketi ya kushiriki Kombe la Dunia nchini Japan mwaka ujao.

Kenya, ambayo haijawahi kushiriki Kombe la Dunia katika historia yake, itaanza kutafita tiketi dhidi ya Canada mnamo Novemba 11, imenyane na Hong Kong mnamo Novemba 17 na kukamilisha kampeni yake dhidi ya Ujerumani hapo Novemba 23.

Itakuwa mara ya kwanza Kenya kukutana na Canada, lakini imewahi kucheza na Ujerumani mara moja na Hong Kong mara sita.

Romania itakuwa mtihani mkubwa kwa Simbas kwa sababu ina ujuzi wa miaka mingi. Imeshiriki Kombe la Dunia tangu makala ya kwanza mwaka 1987, ingawa haitakuwa nchini Japan mwaka 2019 baada ya kuondolewa ilipopatikana imechezesha mchezaji mmoja ambaye si wake katika mechi za kufuzu. Romania inashikilia nafasi ya 17 duniani nayo Kenya ni ya 28.

Vikosi:

Romania A

Wachezaji 15 wa kwanza – Constantin Pristavita, Eugen Capatana (nahodha), Alexandru Gordas, Marius Iftimiciuc, Marian Drenceanu, Adrian Ion, Cristi Chirica, Damian Stratila, Florin Suruglu, Daniel Plai, Ionut Dumitru, Vladut Zaharia, Ionel Melinte

Wachezaji wa akiba – Andre Radoi, Florin Bardasu, Alexandru Savin, Laurentiu Nica, Vasile Balan, Ionut Muresan, Dumani Mtya, Kuselo Moyake, Valentin Calafeteanu, Tudorel Bratu, Tudor Boldor, Alexandru Bucur, Robert Neagu.

Kenya

Patrick Ouko (Homeboyz), Moses Amusala (KCB), Joseph Odero (Kabras Sugar), Hillary Mwanjilwa (Kabras Sugar), Ephraim Oduor (Kabras Sugar), Colman Were (Kabras Sugar), Philip Ikambili (Homeboyz), Oliver Mang’eni (KCB), Wilson K’opondo (Kenya Harlequins), Malcolm Onsando (Kenya Harlequins), Simon Muniafu (Impala Saracens), Andrew Omonde (KCB), George Nyambua (Kabras Sugar), Dalmus Chituyi (Homeboyz), Elkeans Musonye (Strathmore Leos), Joshua Chisanga (Homeboyz), Davis Chenge (KCB), Martin Owilah (KCB), Samson Onsomu (Impala Saracens), Mohammed Omollo (Homeboyz), Samuel Oliech (Impala Saracens), Darwin Mukidza (KCB), Leo Seje Owade (Impala Saracens), Peter Kilonzo (KCB), Collins Injera (Mwamba), Nelson Oyoo (Nakuru), Felix Ayange (Kabras Sugar), William Ambaka (Kenya Harlequins), Tony Onyango (Homeboyz) na William Reeve (Kenya Harlequins).

You can share this post!

Bolt ang’atuka baada ya klabu kudinda kumpa mamilioni...

UPWEKE: Mji wa mtu mmoja pekee

adminleo