• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Wakenya 13 waomba kazi ya kusimamia EACC

Wakenya 13 waomba kazi ya kusimamia EACC

Na BERNARDINE MUTANU

WAKENYA 13 wameorodheshwa kwa mahojiano kujaza wadhifa wa mkurugenzi mkuu wa Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC).

Mahojiano hayo yanatarajiwa kufanyika Novemba 27. Naibu Mkurugenzi Mkuu wa EACC Bw Michael Mubea ni miongoni mwao.

Mahojiano hayo yamepangwa baada ya muda wa kuhudumu wa Halakhe Waqo kukamilika. Bw Waqo amehudumu kwa miaka sita na hana nafasi ya kutuma maombi kuzingatiwa tena kwa nafasi hiyo.

Wengine watakaohojiwa ni Bi Sarah Kilemi, mwanachama wa bodi ya Huduma ya Polisi Murshid Mohamed, Bw James Warui, Bw Vincent Omari, Bw Jillo Kasse, Bw Chege Thenya, Bw Reuben Chirchir, Bw Cyrus Oguna, Bw Abdi Mohamud, Bw Twalib Mbarak, Bw Joel Mabonga na Bi Lucy Wanja.

Bw Waqo aliingia afisini Januari 2013 baada ya EACC kubadilishwa kutoka Tume ya Kitaifa ya Kupambana na Ufisadi (KACC).

Majina ya watakaoorodheshwa yatatumwa bungeni kujadiliwa.

You can share this post!

Mahakama yamkubalia Anne Ngirita kwenda kutibiwa

SHERIA ZA MICHUKI: Wenye matatu walivyogharimika kutii...

adminleo