• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 8:55 PM
FKF yahamisha kambi ya Harambee Stars kutoka Ufaransa hadi Afrika Kusini

FKF yahamisha kambi ya Harambee Stars kutoka Ufaransa hadi Afrika Kusini

Na GEOFFREY ANENE

Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) limepiga breki mipango yake ya kuandalia Harambee Stars kambi ya mazoezi na mechi ya kirafiki nchini Ufaransa hadi pale mwenyeji mpya wa Kombe la Afrika la wanaume (AFCON) atakapojulikana kufikia Desemba 31, 2018.

Katika kikao na wanahabari jijini Nairobi, Rais wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) Nick Mwendwa amesema kwamba Stars itaelekea Ufaransa kombe hili likiandaliwa katika eneo la kaskazini mwa Afrika.

“Majira ya kaskazini mwa Afrika yatakuwa ya joto wakati huo sawa na yale yatakayokuwa Ufaransa wakati huo kwa hivyo hatutakuwa na tatizo kupeleka Harambee Stars nchini Ufaransa. Hata hivyo, Afrika Kusini ikiteuliwa kuandaa makala hayo ya 32, basi tutafutilia mbali kambi ya mazoezi ya Ufaransa pamoja na kusakata mechi za kirafiki barani Ulaya kwa sababu majira yatakuwa baridi nchini Afrika Kusini,” amesema Mwendwa.

Kenya inapanga kusakata kati ya mechi mbili na tatu kabla ya AFCON. Mojawapo ya mechi hizo ni dhidi ya Reggae Boys ya Jamaica jijini London, ambayo imekuwa ikipangwa tangu Februari 2018. Mechi itaondolewa kwenye ratiba ya Kenya ikiwa Afrika Kusini itatwikwa majukumu ya kuandaa AFCON mwaka 2019.

Aidha, Mwendwa alisema kwamba FKF ilitaka Stars ikipige kambi Ufaransa kwa sababu mataifa mengi ya magharibi mwa Afrika hupenda nchi hiyo.

“Itakuwa vigumu sana kuwa na kambi nchini Ufaransa ikiwa Afrika Kusini itachaguliwa kuandaa AFCON kwa sababu ya tofauti hiyo ya majira. Tulitaka kambi hiyo iwe Ufaransa ili tuweze kuzungumza na timu kutoka magharibi mwa Afrika inayoenda AFCON tujipime nayo nguvu ikiwa kambini Ufaransa. Huenda isiwezekane ikiwa Afrika Kusini itachaguliwa kuwa mwenyeji kutokana na tofauti ya majira,” amesema Mwendwa. 

You can share this post!

FUNGUKA: ‘Tunavyosisimua ladha chumbani…’

Kenya yakataa kuandaa AFCON 2019 kutokana na viwanja duni

adminleo