• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Sarafu mpya zitastawisha utalii na kulinda wanyamapori – Balala

Sarafu mpya zitastawisha utalii na kulinda wanyamapori – Balala

Na CHARLES WASONGA

WAZIRI wa Utalii na Wanyama Pori Najib Balala amepongeza hatua ya serikali ya kuweka picha za wanyamapori katika sarafu mpya zilizozinduliwa Jumanne.

Kwenye taarifa aliyoituma kwa vyombo vya habari mnamo Jumatano Waziri Balala alisema sarafu hizo mpya zilizozinduliwa na Rais Uhuru Kenyatta “zinasheheni thamani ya Wakenya na inalingana na kujitolea kwa serikali kustawisha utalii kwa kulinda wanyama pori, mazingira na utamaduni.”

Waziri Balala aliongeza kuwa “picha za wanyama pori hao itakuwa ni kumbukumbu ya kila siku kwamba wanyama hao wana nafasi muhimu katika maisha ya Wakenya.”

“Hii inakumbusha kwamba ni wajibu wetu kuwadumisha na kulinda wanyama hawa kwa manufaa ya vizazi vijavyo,” akasema Waziri Balala.

Mnamo Jumanne Benki Kuu ya Kenya ilizindua sarafa mpya ambazo zinawiana na viwango vilivyowekwa na Katiba. Sarafu hizo hazina picha za marais wa Kenya wa sasa na wa zamani na badala yake zimewekwa picha za wanyamapori.

Sarafu ya Sh5 ina picha ya Kifaru, ya Sh10 ina picha ya simba nay a Sh20 ina picha ya Ndovu. Upande wa pili wa sarafu hizo kuba picha za simba wawili kwenye mchoro wa jina “Harambee” nembo ambayo imekuwepo katika sarafu za zamani.

Akiongoza sherehe ya uzinduzi wa sarafu hizo alipozuru Benki Kuu ya Kenya Rais Uhuru Kenyatta alisema zinaazishia mwanzo mpya wa Kenya katika juhudi za kuijenga kwa kuhifadhi historia yake.

“Sarafu mpya ni njia ya kujijenga, kuhifadhi historia ba utamaduni na kulinda mazingira yetu. Zinaakisi mambo makuu ambayo ni yenye umuhimu mkubwa kwa historia ya nchi hii,” akasema Rais Kenyatta.

Mwanaharakati Okiya Omtata ameishtakiwa CBK kwa kuendelea kutumia safaru zenye picha za marais wa zamani akidai hiyo ni kinyume cha Katiba.

You can share this post!

‘Jaji’ wa kipindi Vioja Mahakamani alivyouawa

Gor wachupa kileleni KPL

adminleo