• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 AM
Mcheza kamari taabani kwa kuwatusi polisi

Mcheza kamari taabani kwa kuwatusi polisi

MCHEZAJI kamari Kennedy Okoth Aete akiwa kizimbani Jumanne kwa kosa la kuwatukana maafisa wa polisi. Picha/RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

MCHEZAJI Kamari aliyeenda  kutafuta riziki katika Jokers Casino jijini Nairobi  alishtakiwa kwa kuwatusi maafisa wa polisi.

Bw Kennedy Okoth Aete alifikishwa mbele ya hakimu mwandamizi Kennedy Cheruiyot, Milimani.

Alikanusha mashtaka mawili dhidi yake.

Alikabiliwa na shtaka la kuzua vurugu kwa lengo la kuhatarisha amani kwa kuwatusi maafisa wa polisi – maneno ambayo hayawezi kuchapishwa.

Bw Aete aliomba aachiliwe kwa dhamana isiyo ya kiwango cha juu.

Aliachiliwa kwa dhamana ya Sh20,000.

You can share this post!

Afisa wa Safaricom aomba msamaha kwa kukosa kumfikisha...

Jaji Odunga apelekwa Machakos majaji 17 wakihamishwa

adminleo