• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:58 PM
Rodriguez ampa kahaba pigo la mwaka

Rodriguez ampa kahaba pigo la mwaka

Na CHRIS ADUNGO

MIPANGO ya kahaba Michele Anne Mason almaarufu ‘Kendra Lust’ kufunga pingu za maisha na nyota wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Colombia, James Rodriguez imetibuka.

Hii ni baada ya fowadi huyo anayechezea Bayern kwa mkopo kutoka Real Madrid kupata hifadhi mpya ya penzi lake moyoni mwa kichuna mzawa wa Urusi, Helga Lovekaty, 26.

Mnamo Julai 2018, Rodriguez alimvisha Kendra Lust pete ya uchumba kwa ahadi ya kumfanya mwanamitindo huyo mkongwe mzawa wa Amerika kuwa wake wa halali.

Kwa mujibu wa gazeti la The Sun, kiini cha Rodriguez kutaka kumfanya Kendra awe wake wa halali ni ugwiji wa kichuna huyo katika sanaa ya kupiga miereka ya chumbani.

Licha ya ukongwe kumtambalia, Kendra mwenye umri wa miaka 41 bado hana kifani katika masuala ya ukahaba na ufundi wa kuwafungulia wanasoka mzinga wake wa asali.

Rodriguez anaanza kuhusiana na Helga baada ya kutemana na mkewe Daniela Ospina aliyedumu naye katika ndoa kwa miaka sita.

Mapema mwezi jana, Rodriguez, 27, alikiri kuvutiwa na ubora wa maumbile ya maziwa kifuani pa Helga ambaye siku hizi ni mwepesi wa kupakia mitandaoni picha anazopigwa kwa pamoja na fowadi huyo.

Baada ya Helga kusifia weledi wa Rodriguez katika upigaji kasia kila aliposhuka kisimani mwake, kichuna huyo kwa sasa analitaka dume lake kukatiza kabisa mawasiliano yake na Kendra.

Licha ya kutalikiana na Daniela, Rodriguez atasalia na jukumu kubwa la kutimiza maslahi yote ya Salome, mtoto ambaye alijaliwa kumpata katika uhusiano wake wa kimapenzi na kipusa huyo, 27.

You can share this post!

TAHARIRI: Mfumo mpya wa elimu uboreshwe

Real Madrid mara hii hawaendi popote UEFA, ManCity wana...

adminleo