• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
Kusafiri Kisumu kwa ndege sasa ni ghali kuliko Mombasa

Kusafiri Kisumu kwa ndege sasa ni ghali kuliko Mombasa

 Na GERALD ANDAE

IDADI kubwa ya watu wanaotumia ndege kusafiri kuelekea Kisumu msimu huu wa krismasi kwa mara ya kwanza imesababisha nauli kupanda kiasi cha kuzidi ile ya kuelekea Mombasa kwa mara ya kwanza.

Watu wanaotumia ndege za Jambojet kuelekea Kisumu wakitoka Nairobi kuanzia jana walilipa Sh14,500, wakati safari za kuelekea Mombasa zitagharimu Sh11,500 msimu huu na kufikia Desemba 24 nauli hiyo itashuka hadi Sh4,500.

Ndege za Fly540 nazo jana kuelekea Kisumu zililipisha Sh11,270.

Wasafiri wa kuelekea Kisumu ka kawaida hulipa kati ya Sh4,500 na Sh6,500 lakini kutokana na kuongezeka kwa watu wanaotafuta huduma hizo sasa bei imepanda, ijapokuwa kwa kawaida nauli za kuelekea Mombasa kwa kawaida huwa juu ya zile za kuelekea huko.

Hata hivyo, nauli za kuelekea mjini Eldoret bado hazijapanda kwani si watu wengi wanatumia ndege kwa usafiri.

Kusafiri kutoka Eldoret hadi Nairobi kwa ndege za Jambojet kati ya Desemba 23 na 24 kutagharimu kati ya Sh9,500 na Sh8,500, kiwango cha juu, hata hivyo, ikilinganishwa na nyakati za kawaida ambapo huwa Sh4,500.

Nauli hizo zilikuwa kulingana na watu waliokuwa wamelipia usafiri kufikia jana, na zinatarajiwa kupanda kadri inavyokaribia krismasi.

Lakini siku ya krismasi yenyewe nauli zitashuka kwani ni watu wachache tu ambao watakuwa wakisafiri wakati huo.

Changamoto ambayo wahudumu wa ndege hizo wamekuwa wakikumbana nazo ni kama kuwafanya Wakenya kukubali kulipia ndege mapema ili kupata usafiri wa bei nafuu.

“Wakenya wanataka kulipia leo wakitaka kusafiri kesho, ama baada ya siku mbili,” akasema afisa wa Jambojet.

Aidha, idadi kubwa ya wasafiri imefanya treni ya SGR kulipiwa hadi Januari.

You can share this post!

Sonko abomoa vyoo, atisha kubomoa hoteli ya Marble Arch

Pasta azaba kidosho kofi kwa kumtongoza

adminleo