• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 8:44 AM
Wakazi Kisii waandamana kukejeli matamshi ya Babu Owino dhidi ya Matiang’i

Wakazi Kisii waandamana kukejeli matamshi ya Babu Owino dhidi ya Matiang’i

Wakazi waandamana mjini Kisii kukashifu matamshi yasiyo na heshima ya mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino dhidi ya waziri wa Usalama wa Ndani Dkt Fred Matiang’i hapo Februari 13, 2018. Picha/ Benson Momanyi

Na JADSON GICHANA

WAKAZI wa Kisii, Jumanne waliandamana kulalamikia matamshi ya mbunge wa Embakasi Mashariki Babu Owino, dhidi ya Waziri wa Usalama Fred Matiang’i.

Walizunguka mitaa ya mji wa Kisii, huku wakiimba nyimbo za kumsifu waziri Matiang’i wakimshutumu kiongozi wa NASA na viongozi wengine katika muungano huo kwa kumkosoa na kumtusi waziri kwa kazi ambayo anafanya.

Walisema kuwa sio vyema kwa upinzani ukiongozwa na Raila Odinga  kwa kumlaumu waziri huyo kwa kufanya kazi yake.

Walizungumza baada ya kukamilisha maandamano hayo wakiongozwa na Enock Mogeni ambaye aliambia upinzani wakome kufanya siasa kwa kila jambo waziri Matiangi anafanya.

Alieleza kuwa wakati huu ni wa serikali kufanya kazi ya kuleta maendeleo kwa wakenya wote.

“Tuko hapa leo kusimama kidete na waziri wetu Dkt Matiang’i kama ndugu yetu. Tumeamua kumuunga mkono afanye kazi yake kwa mujibu wa sheria bila kutishwa na yeyote,” akasema.

“Nimekasirishwa sana na baadhi ya viongozi na wafuasi wao kumtukana na kumkejeli Dkt Matiang’i kwa chochote anapofanya.

Ninawaomba mmpe wakati mwafaka afanyie wakenya kazi,” alisema Bw Mogeni.

 

You can share this post!

Waislamu watakiwa kutumia kondomu

Uzani mdogo wafanya vijana kukataliwa jeshi

adminleo