• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:10 PM
Wakerwa na mhubiri kuwataka waoe kanisani

Wakerwa na mhubiri kuwataka waoe kanisani

Na DENNIS SINYO

MAGEMO, WEBUYE MASHARIKI

WAUMINI wa kanisa moja la eneo hili walitishia kugura kanisa hilo wakidai pasta wao alikataa watu kuoa kwa njia za mkato na kuwataka wafanye harusi.

Kwenye ibada Jumapili, pasta huyo aliwakashifu baadhi ya waumini aliodai walikuwa wakioa kwa njia za mkato. Mhubiri huyo alidai alikuwa amechoka kuitwa kuombea watoto kwenye familia ambazo hakujua wenyewe walivyooana.

Inasemekana aliwaonya waumini ambao hawajaoa kuhakikisha kwamba wanamfahamisha kabla ya kuoa. “Kuanzia leo hakuna mtu hapa atakubaliwa kuoa bila mhubiri kujulishwa. Tunataka tuwe na mpangilio maalum na sio watu kuiba wake za watu, kuwatesa wake na shida ikitokea pasta anaitwa kuingilia kati,” alionya mhubiri huyo.

Maneno hayo hayakuwafurahisha wengi wakisema kuoa ni mapenzi ya mtu na si lazima atangaze.

Jamaa mmoja alisikika akisema kwamba hakuwa na uwezo wa kufanya harusi na atafanya ndoa ya kitamaduni. Alimlaumu pasta kwa kuingilia maisha ya kibinafsi ya watu.

“Kama mtu hana hizo pesa za kufanya harusi, utamlazimisha na hawezi?’ ’aliuliza mama mmoja.

Pasta alisema kanisa lilikuwa likipata aibu kubwa washiriki wake wakioa na kufukuza wake zao jinsi wanavyotaka ilhali kanisa linawashauri waishi kwa amani.

“Sitakubali watu kuoana usiku na mchana wanaachana, ninataka mambo ya wazi watu waishi kwa amani,” alisema pasta huyo.

Inasemekana waumini waliamua kususia hafla za kanisa wakisema tayari pasta alikuwa amewadunisha.
Hata hivyo, waliokuwa wamepanga harusi walifurahia ushauri wa pasta wakisema mambo ya giza hayafai kuruhusiwa kanisani.

 

You can share this post!

Kalonzo ajipata kwa njiapanda: Je, niapishwe? Niondoke...

BI TAIFA VALENTINO DEI 2018

adminleo