• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 6:55 PM
UFISADI: Kesi ya NYS ilivyowaudhi Wakenya 2018

UFISADI: Kesi ya NYS ilivyowaudhi Wakenya 2018

Na RICHARD MUNGUTI

LICHA ya kuwazingira washukiwa wa kashfa ya shirika la Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS) Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) Noordin Haji alikumbana na mawimbi mazito mazito ambayo yalitishia kuzamisha kesi ya Sh226 milioni dhidi ya washukiwa 35.

Miongoni mwa washukiwa hawa ni aliyekuwa katibu mkuu Wizara ya Jinsia Lillian Mbogo Omollo na aliyekuwa Mkurugenzi wa NYS Richard Ndubai.

Washukiwa hawa wanakabiliwa na mashtaka 82 ya matumizi mabaya ya mamlaka na uporaji wa pesa za umma.

Sio tu watumishi wa umma waliotiwa nguvuni pekee bali pia wafanyabiashara ambao kampuni zao zilitumika kufyonza pesa za umma.

Wakurugenzi wa kampuni nne zinazomilikiwa na watu wa familia moja ya Naivasha walishtakiwa pamoja na Bi Omollo , Ndubai na wengine.

Mshukiwa Anne Wambere Ngirita alidaiwa alilipwa zaidi ya Sh50 milioni pasi kutoa huduma zozote kwa NYS.

Anne, dada zake , ndugu yake na mama yao ni miongoni mwa walioshtakiwa katika kashfa hii ambayo viongozi wa mashtaka waliambia mahakama katika taarifa ya utangulizi kuwa Sh8 bilioni zilitoweka katika kashfa hiyo.

 Pia kutoandaa ipasavyo ushahidi katika kesi hiyo ya Sh226 milioni ilifanya mahakama inayoisikiza kulia hoi.

Hata wakati mmoja ilibidi hakimu mkuu Douglas Ogoti na mawakili wanaowatetea washukiwa hao 37  kwa kufilisi NYS kuuliza , “ ni kwa nini ushahidi huu hauajatayarishwa inavyopasa na washukiwa kupewa nakala zao.”

Hakimu alisema tangu aanze kusikiza kesi hiyo amekumbana na vizingiti sio haba ambazo zimemfanya kuiahirishwa kila mara.

Akasema Ogoti: “Kule nje itasemekana kuwa mahakama inachelewesha kesi.Tunalaumiwa bure. Sio mahakimu wanaochelewesha kukamilika kwa kesi.Ni afisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma na ile uchunguzi wa jinai (DCI) zinazoyumbisha kusikizwa kwa kesi hii kwa kutowapa washukiwa nakala za ushahidi.”

Hakimu alidokeza wimbo ambao umekuwa ukikaririwa katika kesi hiyo ni mmoja tu – wa washtakiwa kutopewa nakala za mashahidi.

Washtakiwa na mawakili wao na hakimu wamekuwa wakiuliza swali moja nalo ni hili , “Mbona afisi ya DCI haitaki kuwapa washtakiwa nakala zote za ushahidi uliokusanywa na kurekodiwa kabla ya wao kushikiwa na kufikishwa kortini?”

Ilibainika wazi wazi ni maafisa katika afisi ya DCI ambao wamekawia kuwapa washtakiwa nakala za ushidi waandae utetezi wao.

Katika muda wa zaidi ya mwezi mmoja kesi hiyo imekuwa ikiahirishwa kila inapoanza kusikizwa hata hakimu akasema DPP anakaidi haki za washtakiwa kwa kuchelewa kuwapa nakala za mashahidi.

Kesi hiyo ilipoahirishwa mara mbili ilibidi Bw Ogoti amwagize afisa anayechunguza kesi hiyo kufika mahakamani kuelezea kilichokuwa kinaendelea.

Afisa huyo alifika na kuahidi kuwapa nakala za mashahidi ifikapo Alhamisi.

Haikuwezekana. Punde tu baada ya Bw Sebastian Mokua, shahidi wa kwanza kuingia kizimbani , alichomoa vocha ya malipo kwa makampuni ya Familia ya Ngirita ambao mawakili walisema “ hawajawahi i ona.”

Akiwa amechemka kwa hasira Bw Ogoti alimwuliza kiongozi wa mashtaka Bi Evah Kanyuira , “ Mbona haujawapa washtakiwa nakala za ushahidi huu?”

Bi Kanyuira hakutoa sababu zozote ila kusema “ naomba ushahidi huu uwekwe kando ndipo washtakiwa wapewe nakala zao.”

Baada ya majimbizano ya muda tena ushahidi mwingine wa malipo ya makampuni Njewanga Enterprises na Ngiwaco Enterprises ulichomolewa.

Tena mawakili na hakimu walishangaa sababu ya DPP kuendelea kutoa ushahidi wa kuwatweza mioyo washtakiwa.

Bw Ogoti hakusita kumkemea DPP akisema anakaidi Kifungu nambari 50(2)(J) cha katiba kinachomtaka awape ushahidi wote washukiwa kwa muda unaofaa ndipo waandae ushahidi wao.

“Ukweli uliopo ndio huu, haki za washtakiwa hawa zimekandamizwan na DPP ikiwa kufikia sasa kuna ushahidi ambao hawajapewa,” alisema Bw Ogoti.

Baada ya uzembe wa DPP na DCI wa kutowapa washukiwa ushahidi kujianika adharani, ilibidi Bw Ogoti atoe maagizo mapya kwamba washtakiwa wote wapewe ushahidi.

Ushahidi uliosababisha tumbo joto ulikuwa wa malipo ya Sh19milioni na Sh5milioni mtawalia kwa makampuni ya Njewanga Enterprises na Ngiwaco Enterprises.

Kampuni hizi zinazmilikiwa na Phyilis Njeria Ngirita na Lucy Wambui Ngirita.

Makampuni ya Familia hii ya Ngirita imedaiwa ilipokea mamilioni ya pesa kutoka NYS bila kutoa huduma.

Walioshtakiwa ni Anne Wambere Ngirita, Lucy Wambui Ngirita, Phyilis Njeri Ngirita na ndugu yao Jeremiah Gichini Ngirita.

Aliyekuwa katibu mkuu wizara ya ugatuzi Bi Lillian Omollo ameshtakiwa kuidhinisha malipo ya Sh54.8 milioni kwa Anne, Sh63.2m kwa Lucy , Sh50.9million na Phyilis  na Sh57.8million kwa Jeremiah kinyume cha sheria.

Kesi itaendelea Machi 2019.

You can share this post!

NYS sasa kutegemea mapato yake kujiimarisha

Wakazi wa Nairobi walivyoteswa na Sonko 2018

adminleo