• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 6:55 PM
Wakazi wa Nairobi walivyoteswa na Sonko 2018

Wakazi wa Nairobi walivyoteswa na Sonko 2018

Na RICHARD MUNGUTI

HUKU mwaka wa 2019 ukianza, wakazi wa jiji la Nairobi na wananchi kwa jumla hawatasahau siku walipozuiliwa kushushwa katikati ya jiji kama walivyozea.

Hii ilikuwa baada ya  Gavana Mike Sonko kuamuru magari ya uchukuzi wa abiria yasiingie kati kati mwa jiji kuwashusha na kuwachukua abiria.

Agizo hili liliwakera wengi kwa vile walemavu, kina mama wenye mimba, wakongwe, wagonjwa na wafanyakazi waliwajibika kutembea hadi makazini.

Mbali na kuwachosha wananchi wanaoingia kati kati mwa jiji kufanya na kununua bidhaa za biashara , uchumi uliathirika pakubwa.

Wachanganuzi wa masuala ya kibiashara walikadiria hasara iliyopatikana kufikia zaidi ya Sh3bilioni.

Mahoteli yalipata hasara , mabenki hayakuhudumu ipasavyo na wakazi wengi wa jijini na wale wanaopitia Nairobi wakielekea miji mingine waliteseka.

Lakini Mahakama kuu ilishughulikia kasoro hiyo katika utoaji maagizo na kufutilia mbali agizo hilo la Sonko.

Jaji Wilfrida Okwany alisema kuwa wakazi wa jijini hawakuulizwa maoni yao kabla ya Gavana Sonko kuamuru magari ya uchukuzi yasiingie kati kati mwa jiji.

Jaji Okwany aliratibisha kesi iliyowasilishwa na mfanya biashara na mwanasiasa wa Jubilee Paul Kobia akimshtaki Gavana na kuomba korti irudishe hali ilivyokuwa awali.

Jaji Okwany alisitisha kutekelezwa kwa arifa iliyochapishwa katika Gazeti rasmi yas Serikali mnamo Mei 12 2017 ikipinga kuingia kwa magari ya abiria jijini.

“Katiba inasema lazima maoni ya wananchi yasakwe kabla ya maongozi yanayomwathiri kuchukuliwa,” alisema Jaji Okwany na kuongeza ,” Sonkio hakusaka maoni ya wakazi wa jijini. Agizo hilo la kuzuia magari kuingia kati kati mwa jiji linakinzana na katiba.”

Jaji huyo aliamuru Bw Kobia amkabidhi Sonko nakala za kesi aliyomshtaki ndipo awasilishe majibu.

Akipokea ushahidi kutoka kwa Bw Kobia , Jaji Okwany alielezwa wiki iliyopita Bw Sonko aliamuru arifa ya magari ya matatu kutoingia kati kati mwa jiji la Nairobi kuwachukua abiria na kuwashusha ianze kutekelezwa.

“Mnamo 2011 , Bw Sonko alifaulu kusitisha kutekelezwa kwa arifa sawa na hii iliyochapishwa na lililokuwa baraza la jiji la Nairobi la kuzuia magari ya uchukuzi wa abiria kuingia jijini,” Jaji Okwany alifahamishwa.

Jaji huyo aliambiwa Mahakama kuu ilisitisha kutekelezwa kwa agizo hilo.

“Kabla ya kutekelezwa kwa agizo hilo , Bw Sonko , Serikali ya kaunti ya Nairobi na Polisi (NPS) hakukuwa na mipango kabambe jinsi abiria wakishushwa nje ya kati kati mwa jiji watakavyosafiri kuingia kati kati mwa jiji,” aliteta Bw Kobia.

Bw Kobia aliteta kuwa umma haukuulizwa maoni yake kabla ya kutelezwa kake.

Kabla ya Bw Kobia kumshtaki Sonko vyama 22 vya magari ya uchukuzi wa abiria yalimshtaki yakiomba agizo hilo lisitishwe. Lakini Jaji Pauline Nyamweya hakuisitisha kutekelezwa kwa agizo hilo magari ya matatu yasibebe abiria ama kuwashusha kati kati mwa jiji la alikataa kusitisha kutekelezwa kwa agizo kwamba magari yote ya Matatu yawashushe abirie nje ya eneo la kati kati mwa jiji (CBD) kupunguza msongamano.

Na si hii kesi tu wakili Boniface Nyamu aliwasilisha kesi ya kumtimua Sonko mamlakani kwa kukaidi katiba na sheria.

Bw Nyamu anadai Bw Sonko ameshindwa kumteua naibu wake na huenda kaunti hii ikatumbukia nyongo endapo kwa njia moja au nyingine akumbwe na matitizo.

Jaji Okwany aliratibisha kesi hii kuwa ya dharura.

 

You can share this post!

UFISADI: Kesi ya NYS ilivyowaudhi Wakenya 2018

Aponea kifo baada la kutumbukia ndani ya Mto Ngong akivuta...

adminleo