• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Chebii kutetea taji la Lake Biwa Mainichi Marathon, Japan

Chebii kutetea taji la Lake Biwa Mainichi Marathon, Japan

Na GEOFFREY ANENE

MKENYA Ezekiel Chebii amethibitisha atatetea taji la Lake Biwa Mainichi Marathon nchini Japan hapo Machi 4, 2018.

Chebii, 27, anajivunia muda bora kuliko wapinzani wake katika mbio hizi za kilomita 42 wa saa 2:06:07 aliotimka mjini Amsterdam nchini Uholanzi mwaka 2016.

Mahasimu wake wakuu ni Mswizi Tadesse Abraham, 35, na Muethiopia Abera Kuma, ambao walitimka muda wao bora wa saa 2:06:40 na 2:05:56 mwaka 2016 na 2014, mtawalia. Watatu hawa wanapigiwa upatu kutwaa taji la mwaka 2018.

Hata hivyo, kuna wakimbiaji wengine ambao hawawezi kupuuzwa. Wakimbiaji hao ni bingwa wa Gold Coast Marathon mwaka 2017 Takuya Noguchi, Satoru Sasaki, Takuya Fukatsu, Fumihiro Maruyama, Kenta Murayama, Asahi Kasei na Masato Imai (wote kutoka Japan).

Jake Robertson (New Zealand) na mkazi wa Japan, Macharia Ndirangu (Kenya) wanakamilisha orodha ya wakimbiaji wanaoweza kushinda makala haya ya 73.

Daniele Meucci (Italia), Cristhian Pacheco (Peru), Mohammed Zani (Morocco), Samson Gebreyohannes (Eritrea) na Mkenya Michael Githae (Kenya) pia wako katika orodha ya washiriki watajika.

You can share this post!

UEFA Valentino Dei: KTN Home kuonyesha Liverpool ikivaana...

Wakenya wafukuza donge nono Diamond League, wakwepa Jumuiya...

adminleo