• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 5:46 PM
Polisi wapinga ripoti wamewapa silaha maafisa wa akiba

Polisi wapinga ripoti wamewapa silaha maafisa wa akiba

Na PETER MBURU

IDARA ya Huduma za Polisi (NPS)imepinga vikali ripoti kutoka kwa gazeti la The Star kuwa imekuwa ikiwahami maafisa wa polisi wa akiba (KPR), ikitaja habari hiyo kuwa ya wongo na ya kupotosha.

Idara hiyo ilisema kuwa haijawapa silaha wala kuajiri kisiri maafisa wowote wa KPR, ikisema ripoti ya gazeti hilo inatishia kuvuruga amani katika jamii ambapo kikosi hicho hufanya kazi.

Aidha, idara hiyo kupitia akaunti yake ya Twitter ilisema kuwa maafisa wa KPR ambao imeajiri wanajulikana na wakazi ambapo wanahudumu.

“Habari hiyo ni mchanganyiko wa ukweli mchache na uongo mwingi ambao unaleta shaka isiyohitajika miongoni mwa watu. Tunarai umma kupuuza habari hiyo,” idara ya NPS ikasema.

Ilisema kuwa habari yenyewe inaweza kuwa na hatari ya kujenga mjadala kuwa kuna haja ya kupunguzwa kwa maafisa wa kikosi hicho, wakati kwa kweli wanahitajika kwa wingi.

“Tunashauri kuwa haki ya wanahabari kueleza matukio yanayoendelea haifai kutumiwa vibaya kwa kuchapisha habari zisizo za kweli,” NPS ikaasema.

Ilipinga madai kuwa kuna mwingilio wa kisiasa katika shughuli ya kuwaajiri maafisa wa KPR, ikisema “uajiri wa maafisa hao hauhusiani kisiasa kwa njia yoyote.”

“Tunapanga kuongeza idadi ya maafisa katika meneo ambapo wizi wa mifugo umekita,” polisi wakaongeza.

Walisema kuwa hadi sasa, kikosi hicho kina maafisa 11,000 katika maeneo ya kaskazini mwa Bonde la Ufa na Kaskazini Mashariki mwa Kenya, ambao wamechangia kupungua kwa visa vya ukora na wizi wa mifugo katika maeneo hayo.

“NPS haihusiki na haifanyi kitu chochote kinachohusiana na kuhami kisiri maafisa wa KPR na wale walioajiriwa wanajulikana vyema na wakazi wa maeneo ambapo wanahudumu,” ikasema idara hiyo.

You can share this post!

Pendekezo la Moses Kuria kuhusu sheria za uchaguzi

Hofu mpya kuhusu madeni ya Uchina

adminleo