• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 AM
UTAMADUNI: Watu milioni 15 kukongamana katika mito mitakatifu

UTAMADUNI: Watu milioni 15 kukongamana katika mito mitakatifu

MASHIRIKA Na PETER MBURU

TAYARI watu milioni 4 wameanza kushiriki utamaduni wa kukongamana majini nchini India, baada yao kwenda katika mito mitakatifu ya Ganges na Yamuna, kuadhimisha hafla ya Kumbh Mela, ambayo ndiyo huwa mkutano mkubwa zaidi wa watu duniani.

Angalau watu milioni 15 wanatarajiwa kuhudhuria katika siku yake ya kwanza pekee, huku katika kipindi kizima cha hafla hiyo ambacho kitakuwa siku 49 kikitarajiwa kuvuta watu milioni 120.

Jamii ya Hindu ina Imani kuwa kuoga katika mito hiyo kutawasaidia kuosha thambi zao na kupata wokovu.

Wanaume watakatifu ndio walikuwa wa kwanza kuwasili kwa hafla hiyo mapema Jumanne, ambapo walijipaka jivu milini na kwenda majini wakiimba, kucheza densi na kupiga picha.

Wakati wa hafla hiyo mnamo 2013, wanawake watakatifu kwa mara ya kwanza katika historia waliruhusiwa kuoga katika maji hayo. Mwaka huu, hata watu wa jinsia mbili waliruhusiwa kushiriki.

“Maandalizi ya mwisho yanaendelea, vikundi vyote vya kidini vimetengewa wakati na nafasi ya kutekeleza utamaduni huo,” akasema Rajeev Rai, afisa mkuu wa usimamizi.

Utamaduni huo umekuwa ukiendeshwa kwa karne nyingi, lakini kwa miongo miwili iliyopita imekua na kubadilika kuwa hafla inayounganisha watu wengi zaidi.

You can share this post!

KENYA IMARA: Mashujaa walivyowazidi nguvu magaidi

SHAMBULIO: Wakenya waonyesha umoja baada ya uvamizi

adminleo