• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Mtoto wa miaka 4 ampiga mamake mjamzito risasi

Mtoto wa miaka 4 ampiga mamake mjamzito risasi

MASHIRIKA Na PETER MBURU

MTOTO wa miaka minne kutoka Marekani alimpiga mamake mja mzito risasi wakati alipopata bunduki chini ya godoro,  na kumwacha na jeraha.

Msemaji wa polisi eneo la King County Ryan Abbott alitaja kisa hicho cha kiajali, akisema kuwa mamake mtoto huyo ambaye ana ujauzito wa miezi minane ametibiwa, baada ya kukimbizwa katika hospitali moja na majeraha mabaya.

Mtoto huyo alikuwa katika chumba cha kulala Jumamosi alasiri wakati alipata bunduki hiyo iliyokuwa na risasi na bila kufahamu alichokuwa akifanya akampiga mamake risasi.

Baba na mamake mtoto huyo walikuwa wamelala kitandani wakati huo.

“Aliipata bunduki na kumpiga mamake risasi usoni,” akasema Abbott.

You can share this post!

Shughuli nyingi zinazoisubiri Bunge kuanzia Februari 12

Kuua wanawake 5 kulinifanya nijihisi mkamilifu, asema...

adminleo