• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:05 AM
UG sasa kutumia wanawake warembo kuvutia watalii

UG sasa kutumia wanawake warembo kuvutia watalii

DAILY MONITOR Na PETER MBURU

SERIKALI ya Uganda kupitia Wizara ya Utalii imeamua kuwatumia wanawake wenye mili ya kuvutia na umbo mduara kama kivutio cha watalii wa kigeni.

Waziri wa Utalii nchini humo Godfrey Kiwanda alianzisha shindano la urembo la ‘Miss Curvy Uganda’ Jumanne kama hatua ya kuinua utalii wa taifa hilo.

Wanawake wanaojiamini kuwa warembo wanatarajiwa kushindana kuhusu yupi mrembo na mwenye makalio ya kuvutia, kisha baadae mshindi washindi watakaotumika kuvutia watalii watangazwe mnamo Juni.

Waziri huyo alianzisha shindano hilo katika hoteli moja Jiji kuu la Kampala, wakati alipeperusha bendera huku wanawake waliovalia mavazi ya kubana wakizunguka kando ya kidimbwi cha kuogelea, wakipigwa picha na waandalizi wa shindano hilo.

“Tumekuwa tukiwatuza wanawake wanaovutia na ambao ni warembo kuangaliwa kila siku. Kwanini tusiwatumie kama mbinu ya kuinua utalii wetu?” Bw Kiwanda akasema.

Sekta ya Utalii ndiyo huipatia nchi ya Uganda pesa nyingi zaidi za kigeni, kwani mwaka uliopita ilipata zaidi ya S100milioni (za Kenya), kulingana na rekodi za serikali.

Watalii wengi huzuru mbuga kutazama wanyama na ndege, mbali na ziwa Victoria ambalo ndiyo chemichemi ya Mto Nile.

Lakini sasa Uganda imeamua kupanua nyanja za kupata hela zaidi za kigeni, sasa kwa kuongeza bidhaa nyingine katika menyu ya utalii, wanawake wenye makalio ya kuvutia na warembo kabisa.

Mwandalizi mkuu wa shindano hilo la urembo Ann Mungoma alisema kuwa ana matumaini kuwa litawaangaza watu wa Uganda na kuwafanya kuvutia ulimwengu.

“Ni shindano ambalo litaonyesha urembo halisi wa mwanamke Mwafrika. Litawafanya wanawake wa umri mdogo kuonyesha weledi na makalio yao ya kuvutia,” akasema Bi Mungoma.

Watakaohusika katika shindano hilo, hata hivyo, ni wale wa kati ya umri wa miaka 18 na 35 pekee, wengine wakifungiwa nje.

You can share this post!

Wanachuo watakiwa kuwa wabunifu baada ya masomo

Waliompa ajuza wa miaka 83 bangi wasakwa

adminleo