• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:21 PM
Dhuluma za kimapenzi dhidi ya watoto zikomeshwe – Wabunge wanawake

Dhuluma za kimapenzi dhidi ya watoto zikomeshwe – Wabunge wanawake

Na CHARLES WASONGA

WABUNGE wanawake Jumatano wameshtumu kuongezeka kwa visa vya dhuluma za kimapenzi dhidi watoto wakiapa kuandamana katika kaunti ya Nandi .

Kwenye kikao na wanahabari katika majengo ya bunge Jumatano, wabunge hao watatu wakiongozwa na Mbunge Mwakilishi wa kaunti ya Nandi Dkt Tecla Tum wameshtumu kitendo ambapo naibu mmoja wa chifu katika kaunti hiyo alimdhulumu kimapenzi mtoto, na kuitaka serikali kumwadhibu afisa huyo wa utawala

“Ili kuonyesha ghadhabu yetu kama viongozi kina mama, nitaongoza maandamano Ijumaa kupinga kitendo hicho cha kikatili dhidi ya wasichana,” akasema Dkt Tum.

Alikuwa ameandama na wenzake; Gladys Shollei (Uasin Gishu) na Florence Bore Tapnyole (Kericho).

Dkt Tum alisema mtoto wa kike aliyedhulumiwa anapokea matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Nandi, mjini Kapsabet.

Kufikia sasa, idadi ya watoto wa kike ambao wamedhulumiwa katika kaunti hiyo ni 10 huku ikihofiwa kuwa huenda idadi ikawa juu kwa sababu kuna visa vingi ambavyo huwa haviripotiwi.

Dkt Tum amewataka wazazi wa wahasiriwa kukoma kusuluhisha visa hivyo nje ya mahakama akishauri kuwa sheria inapasa kufuata mkondo wake.

You can share this post!

Serikali ilipe bili za wagonjwa wanaofariki wakitibiwa...

Msitarajie nyongeza ya mshahara, serikali haina hela...

adminleo