• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 10:10 AM
Atwoli anagawanya jamii ya Abaluhya, aonya Wetang’ula

Atwoli anagawanya jamii ya Abaluhya, aonya Wetang’ula

Kinara wa muungano wa NASA na kiongozi wa chama cha Ford Kenya Bw Moses Wetang’ula. Picha/ Maktaba

Na LEONARD ONYANGO

KINARA mwenza wa muungano wa NASA Moses Wetang’ula ameitaka jamii ya watu wa Magharibi kupuuzilia mbali Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi (Cotu) Francis Atwoli huku akisema kuwa analenga kugawanya jamii ya Waluhya.

Bw Wetang’ula alimshambulia Bw Atwoli saa chache baada ya kiongozi huyo wa Cotu kutangaza Jumapili kwamba kiongozi wa chama cha Amani National Congress (ANC) ambaye pia ni kinara mwenza wa NASA Musalia Mudavadi ataendelea kuwa msemaji wa jamii ya Waluhya.

Bw Atwoli alisema kwamba amemsamehe Bw Mudavadi, kwa kuhepa hafla ya kumuapisha kiongozi wa muungano huo Raila Odinga mnamo Januari 30, 2018.

Bw Mudavadi, Bw Wetang’ula na kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka walisusia hafla ya kuapishwa Bw Odinga kuwa ‘rais wa wananchi’.

Bw Atwoli aliyesema hayo baada ya mkutano wa faragha nyumbani kwa  Bw Mudavadi alisema: “Tumekubaliana kwamba Bw Mudavadi ataendelea kuwa msemaji wa jamii ya Waluhya bila kutatizwa na yeyote.”

Lakini matamshi hayo yalimkera Seneta wa Bungoma Wetang’ula huku akiyataja kuwa ‘sarakasi’.

“Sarakasi za Atwoli hazitasaidia kwa lolote kuunganisha jamii ya Waluhya na badala yake anatugawanya,” akasema Bw Wetang’ula kupitia Twitter.

“Mbona Bw Atwoli anaangazia Mudavadi kwani hakuna Waluhya waliochaguliwa katika maeneo Bungoma, Trans Nzoia naNairobi?” akauliza Bw Wetang’ula.

You can share this post!

Onyo Nzoia Sugar yaweza kushushwa daraja

KRA yapoteza mabilioni kutokana na bidhaa ghushi

adminleo