• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 1:51 PM
Bwanyenye akana mashtaka mapya

Bwanyenye akana mashtaka mapya

Bwanyenye Mohan Galot (kulia) na mkewe walipofika katika mahakama ya Milimani JumatatU. Picha/RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

BWANYENYE Mohan Galot na mkewe walifikishwa katika mahakama ya Milimani wakikabiliwa na mashtaka ya kughushi cheti cha kuandikisha kampuni ya Galot Industries akidai ni halali.

Shtaka lasema Mohan  Galot alighushi cheti hicho mnamo Agosti 5 2016 akidai kilitolewa na Msajili wa Kampuni katika afisi ya mwanasheria mkuu Bw Nicholas Oduor.

Mawakili Kirathe Wandugi na Prof Tom Ojienda walipinga Bw Galot akisomewa mashtaka na kuyajibu waLisema, “upande wa mashtaka unatumia kitengo cha mahakama kwa njia mbaya.”

Mawakili hao walimshambulia kiongozi wa mashtaka Daniel Karori na maafisa wa polisi wanaochunguza kesi dhidi ya Bw Galot wakisema “afisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma ilikuwa inafanya mchezo wa paka na panya.”

Bw Wandungi alisema wamejulishwa na wanahabari kuhusu mashtaka mapya dhidi ya Bw Galot.

Hakimu mkuu Francis Andayi aliamuru mashtaka hayo mapya dhidi ya Bw Galot yasisomwe hadi wakati mwingine.

Na wakati huo huo Bw Andayi akawaruhusu Mabw Wandugi na Prof Ojienda kuendelea kuwatetea wanaohusika na kesi hiyo.

You can share this post!

KRA yapoteza mabilioni kutokana na bidhaa ghushi

Rais hafai kukosolewa akiteua mawaziri – Mahakama

adminleo