• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 4:01 PM
Omtatah amletea matata wakili Ogeto

Omtatah amletea matata wakili Ogeto

Wakili Kennedy Ogeto aliyeteuliwa kuwa wakili mkuu wa Serikali na Rais Uhuru Kenyatta. Picha/ RICHARD MUNGUTI

Na RICHARD MUNGUTI

MWANAHARAKATI Okiya Omtatah Jumatatu aliwasilisha kesi katika mahakama kuu kupinga uteuzi wa wakili Kennedy Ogeto kuwa wakili mkuu wa Serikali.

Katika kesi aliyowasilishwa katika mahakama kuu ya Milimani Nairobi Bw Omtatah alisema Rais Uhuru Kenyatta alikaidi katiba alipomteua Bw Ogeto katika wadhifa huo wa umma.

Mwanaharakati huyo amesema Rais Kenyatta alikaidi katiba kwa kumteua Bw Ogeto kuwa wakili mkuu wa Serikali kabla ya kutangaza nafasi katika afisi hiyo.

Bw Ogeto aliteuliwa kutwaa wadhifa huo baada ya aliyekuwa wakili mkuu wa Serikali Bw Njee Muturi kupelekwa kuwa naibu wa mkuu wa wafanyakazi katika Ikulu.

Bw Omtatah amesema hakuna mahojiano yaliyofanywa kuona iwapo Bw Ogeto amehitimu.

Kabla ya kuteuliwa Bw Ogeto alikuwa mmoja wa mawakili waliomwakilisha Rais Kenyatta katika kesi ya kupinga uchaguzi wake Agosti 8 na Oktoba 26 2017.

Tena alikuwa anamwakilisha Rais Kenyatta katika kesi mahakama ya kimataifa ya uhalifu (ICC) aliposhtakiwa kufuatia ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007/2008 ambapo watu zaidi ya 1,000 waliuawa na wengine zaidi ya 600,000 kufurushwa makwao.

Mbali na kesi hii dhidi ya Bw Ogeto , Bw Omtatah amemshtaki pia Rais Kenyatta kwa uteuzi wa mawaziri.

You can share this post!

Rais hafai kukosolewa akiteua mawaziri – Mahakama

Wawili wakana kuiba Sh50 milioni hospitali ya Mater

adminleo