• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Wawili wakana kuiba Sh50 milioni hospitali ya Mater

Wawili wakana kuiba Sh50 milioni hospitali ya Mater

Solomon Odeny (kulia) na Paul Oming’o katika mahakama ya Milimani waliposhtakiwa kwa kuibia hospitali ya Mater zaidi ya Sh50 milioni. Picha/ Richard Munguti

Na RICHARD MUNGUTI

MHASIBU na mfanyakazi katika kampuni ya mawasiliano ya Wananchi Telecom walikanusha mashtaka mawili ya kuibia pesa hospitali ya Mater miaka 11 iliyopita.

Solomon Odeny na Paul Oming’o walishtakiwa mbele ya hakimu mwandamizi Bi Martha Mutuku.

Walikana kati ya Aprili 3, 2006 na Januari 31, 2017 jijini Nairobi wakishirikiana na watu wengine ambao hawajashtakiwa waliiba kitita cha Sh50,143,948 mali ya hospitali ya Mater Misericordiae.

Shtaka la pili dhidi ya Bw Oming’o lilisema kuwa kati ya Julai 22, 2012 na September 2, 2016 aliiba Sh29,997,514 alipokuwa ameajiriwa kama mhasibu na hospitali hiyo ya Mater.

Waliachiliwa kwa dhamana ya Sh500,000 pesa tasilimu hadi Juni 6, 2018 kesi itakaposikizwa.

You can share this post!

Omtatah amletea matata wakili Ogeto

Yatima asukumwa rumande kuhusu wizi wa Sh2.5 milioni

adminleo