• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 4:36 PM
Miguna Miguna arudishwe nchini, mahakama yaamuru

Miguna Miguna arudishwe nchini, mahakama yaamuru

Mawakili Nelson Havi (kulia) na Cliff Ombeta wateta kuhusu ukaidi wa maafisa wakuu serikali kutotii maagizo ya korti. Picha/RICHARD MUNGUTI

RICHARD MUNGUTI

KIZAAZAA cha kumfurusha mwanaharakati na kiongozi wa vuguvugu la National Resistany Movement (NRM) la muungano wa Nasa, Dkt Miguna Miguna, kiliendelea kutifuka Alhamisi baada ya Mahakama Kuu kuamuru arudishwe Kenya kutoka Canada.

Jaji Luka Kimaru aliamuru Dkt Miguna arudishwe Kenya kwa vile Serikali ilikaidi agizo la korti mwanasheria huyo mbishi na mwenye matata afikishwe kortini.

Jaji Kimaru alisema hatua ya serikali kumfurusha Miguna ni kinyume cha katiba na sheria za kimataifa zinazosema kuwa mmoja hawezi kupokonywa uraia wake.

Miguna ni mzaliwa wa eneobunge la Nyando, kaunti ya Kisumu lakini alipata uraia wa Canada alipoenda kupokea masomo ya juu.

Mawakili Cliff Ombeta na Nelson Havi waliomba agizo hilo la Serikali lifutiliwe mbali na Miguna arudishwe nchini.

Jaji Kimaru alisitisha kuwachukulia hatua kali wakuu wa Polisi Joseph Boinnet na George Kinoti ndipo wamrudishe Miguna nchini kuendelea na kesi aliyoshtakiwa na aliuyoshtaki.

You can share this post!

Yatima asukumwa rumande kuhusu wizi wa Sh2.5 milioni

Ndege nne za Jambojet kuimarisha safari Afrika

adminleo