• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 5:29 PM
Mkaguzi mkuu sasa yuko huru kukagua hesabu za KDF

Mkaguzi mkuu sasa yuko huru kukagua hesabu za KDF

Na BERNARDINE MUTANU

MKAGUZI mkuu wa hesabu za serikali amepewa idhini ya kukagua matumizi ya mabilioni ya fedha zilizotolewa kwa jeshi na taasisi zingine za usalama nchini.

Idhini hiyo ilitolewa na Mahakama Kuu baada ya Jaji Chacha Mwita kusema kuwa Sehemu 40 ya Ukaguzi wa Matumizi ya Fedha za Umma (2015) na sehemu zingine za sheria hiyo haikuambatana na Katiba.

Kulingana na sehemu hiyo, wahusika wa ufisadi katika taasisi hizo wanaweza kukingwa. Lakini baada ya uamuzi huo wa Jaji Chacha, inamaanisha kuwa yuko huru kukagua matumizi ya kifedha katika Shirika la Upelelezi (NIS), jeshi (KDF) na Huduma ya Kitaifa ya Polisi.

Kulingana na jaji huyo, sheria hiyo na zingine nane, ziliingilia uhuru wa Kikatiba wa Afisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali.

Sehemu hizo ni 4(2), 8, 12, 17(1), 18, 27, 40, 42 na 70, ambazo zaidi alisema zilikuwa kinyume cha kanuni na mwongozo uliotolewa na Katiba.

You can share this post!

KCB, Equity na Co-operative zashushwa na Moody’s

NYS yapewa ekari 100,000 kukuza pamba Galana-Kulalu

adminleo