• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 6:47 AM
IEBC yasema inahitaji Sh8 bilioni kutathmini upya mipaka

IEBC yasema inahitaji Sh8 bilioni kutathmini upya mipaka

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini (IEBC) Bw Wafula Chebukati. Utathmini wa mipaka utafanyika baada ya hesabu ya watu ya 2019. Picha/ Maktaba

Na BERNARDINE MUTANU

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini (IEBC) inahitaji Sh8 bilioni kutathmini mipaka ya maeneobunge na wadi kwa mara ya pili.

Kulingana na mwenyekiti wa IEBC Bw Wafula Chebukati, tathmini inafaa kufanyika kati ya Februari na Agosti 3, 2021.

Alisema hayo alipofika mbele ya Kamati ya Bunge kuhusu Utekelezaji wa Katiba inayosimamiwa na Bw Jeremiah Kioni, Mbunge wa Ndaragwa.

Kulingana na Bw Chebukati, watategemea data kutoka kwa ripoti kuhusu idadi ya watu nchini inayotarajiwa kutolewa mwaka  2019.

Kulingana na kifungu cha 89 cha Katiba, IEBC inafaa kutathmini mipaka kati ya miaka nane na miaka 12 na tathmini inafaa kukamilika mwaka mmoja kabla ya uchaguzi wa ubunge kufanywa.

Itakuwa tathmini ya kwanza tangu Katiba mpya kuzinduliwa 2010. Mipaka ya maeneobunge na wadi iliundwa kwa kufuata katiba hiyo.

You can share this post!

NYS yapewa ekari 100,000 kukuza pamba Galana-Kulalu

Gharama ya umeme kupanda zaidi kusiponyesha

adminleo