• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Banglandesh yazima tovuti 20,000 za ngono

Banglandesh yazima tovuti 20,000 za ngono

MASHIRIKA Na PETER MBURU

SERIKALI ya Bangladesh imezima takriban tovuti 20,000 ambazo zimekuwa zikipeperusha mambo ya ngono na michezo ya kamari, kama sehemu ya operesheni ya kumaliza biashara hiyo, waziri amedhibitisha.

Watoaji wa huduma za intaneti wiki iliyopita waliondoa tovuti zote ambazo zinatoa huduma za Kamari ama kanda za ngono, baada ya kuamrishwa na mamlaka ya kudhibiti mitandao ya mawasiliano nchini humo.

“Nataka kuwe na intaneti salama na safi kwa raia wote wa Bangladesh, ikiwemo watoto. Na hivi ni vita vyangu dhidi ya mitandao ya ngono na vitakuwa vita visivyoisha,” akasema Mustafa Jabbar, waziri wa mawasiliano.

Mitandao ya kijamii kama TikTok na Bigo ambayo ina umaarufu mkubwa nchini humo- na ambayo serikali inaamini imekuwa ikitumiwa vibaya- aidha ilizimwa, Bw Jabbar akadhibitisha.

Mitandao mingi iliyozimwa imekuwa ikiendeshwa kutoka nje ya nchi hiyo, japo mingine pamoja na ile ya kijamii imekuwa ikiendeshwa kutoka ndani ya mipaka yake.

Operesheni hiyo ilianzishwa baada ya Mahakama Kuu ya nchi hiyo Novemba mwaka uliopita kuamrisha tovuti za ngono kupigwa marufuku na kuzimwa.

Korti ilitoa uamuzi huo baada ya shirika la kutetea haki kufika kortini, likisema kuwa mitandao mingi ilikuwa ikichapisha mambo ya kupotosha kimaadili.

“Tunachunguza kurasa za Facebook za humu nchini, mitandao ya Youtube na tovuti pia,” akasema Bw Jabbar.

“Chache zimezimwa kwa kuwa na mambo yasiyokubalika kimaadili. Tumeshauri watu wengine kutochapisha kitu chochote ambacho kinakiuka maadili yetu ya kijamii,” akasema.

Bangladesh kuna zaidi ya raia milioni 160 na asilimia 90 yao ni watumizi wa intaneti. Masuala ya ngono yamekuwa yakiongoza kitu ambacho raia wa nchi hiyo wanatumia kwenye intaneti sana.

You can share this post!

Wanasayansi sasa wadai bangi inaongeza nguvu za kiume

Azpilicueta lawamani Kepa kukaidi Sarri kwa fainali

adminleo