• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 5:22 PM
Kenya kupokea mkopo mwingine wa Eurobond wa Sh200 bilioni

Kenya kupokea mkopo mwingine wa Eurobond wa Sh200 bilioni

Na LEONARD ONYANGO

SERIKALI imetangaza kuwa imefanikiwa kupata mkopo mpya wa Sh203 bilioni wa Eurobond.

Waziri wa Fedha Henry Rotich alisema fedha hizo zitatumiwa katika miradi ya ujenzi wa miundomsingi na kulipa madeni mengineyo.

“Tutaendelea kuwekeza katika ujenzi wa miundomsingi na miradi mingineyo ya maendeleo,” akasema Waziri Rotich kupitia taarifa yake kwa wanahabari.

Rais Uhuru Kenyatta alisema mafanikio ya mkopo huo ni ishara kuwa wawekezaji wa kimataifa wana imani na uchumi wa Kenya.

Mkopo wa Eurobond mnamo 2016, uliibua mjadala mkali kuhusiana na matumizi yake huku kiongozi wa upinzani Raila Odinga akidai kuwa fedha hizo ziliibwa na baadhi ya maafisa wakuu serikalini.

Mnamo Mei 2016, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma Keriako Tobiko alisema kuwa hakukuwa na ushahidi wa kuonyesha kuwa fedha hizo ziliporwa.

Afisi ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali Edward Ouko kufikia sasa imeshindwa kutegua kitendawili kuhusiana na fedha hizo.

You can share this post!

Madeni ya vipodozi yamaliza ndoa yake

BI TAIFA FEBRUARI 21, 2018

adminleo