• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Gor yafuzu kwa raundi ya pili CAF

Gor yafuzu kwa raundi ya pili CAF

Na CECIL ODONGO

KLABU ya Gor Mahia imefuzu kwa raundi ya pili ya kufuzu kwa mchuano wa ubingwa wa bara Afrika, CAF.

 Mabingwa hao wa ligi ya KPL walifuzu kwa jumla ya mabao 3-1 baada ya kuagana sare ya 1-1 na Klabu ya Leones Vegetarianos ya Equitoria Guinea. Mkondo wa kwanza ulishuhudia Gor wakiwabamiza mabao 2-0 uwanjani Machakos.

Kwenye mchuano huo  wenyeji walichukua uongozi  katika dakika sitini na walihitaji kuongeza bao moja tu ili mchuano huo uamuliwe kwa penalty lakini hilo halikutimia.

K’ogalo walizidisha mashambulizi na kupata bao dakika za majeruhi baada ya kona uliochanjwa vizuri na Francis Kahata kujazwa wavuni na mchezaji wa Klabu hiyo.

Matokeo hayo sasa yanaiweka Gor katika ulazima wa kukutana na mabingwa wa ligi nchini Tunisia,Esperance. Mechi ya mkondo wa kwanza utachezwa hapa nchini.

Esperance waliwafunga Gor jumla ya mabao 8-2 kwenye  mikondo yote miwili mwaka wa 2014 walipokutana kwenye kipute hicho.

  • Tags

You can share this post!

Gor kuvaana na Kariobangi huku Ingwe ikikabiliana na Ulinzi

Familia ya Voi yapeleka maiti kwa duka la mtu wanayedai...

adminleo