• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 10:55 AM
Mwanamke ampiga risasi mpenzi wake kwa kukoroma usingizini

Mwanamke ampiga risasi mpenzi wake kwa kukoroma usingizini

MASHIRIKA Na PETER MBURU

MWANAMKE kutoka Florida, Marekani amefunguliwa mashtaka ya kujaribu kuua, baada ya kumpiga mpenzi wake risasi, walipokuwa wakibishana kuhusu hali yake ya kukoroma wakati anapolala.

Idara ya polisi Kaunti ya Brevard ilisema kuwa Lorie Morin, 47 alikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya kujaribu kuua, baada ya kumpiga risasi mpenzi wake wa wiki tatu, kwa kuwa alikuwa akikoroma kwa sauti ya juu wakati wa kulala.

Polisi walifahamishwa kuhusu kisa hicho Jumatano wiki iliyopita, japo wote mshukiwa na mpenzi wake walikiri kuwa hakupiga risasi kwa kutaka, ili ilikuwa kimakosa.

Baadaye polisi walibaini kuwa mwanamke huyo alichochewa kumpiga mpenziwe risasi na ugomvi uliokuwa ukiendelea baina yao, kuhusu hali ya mwanamume huyo kukoroma, kwa sauti kubwa sana.

Nakala za korti zinaonyesha kuwa mwanamume huyo alikuwa amemtembelea mshukiwa usiku huo, huku ijapokuwa Morin alitarajia angekuwa na usiku mtulivu, ukageuka kuwa wa kelele si haba, kufuatia hali yake ya kukoroma sana.

“Wote walikuwa wakinywa pombe kabla na wakati wa ugomvi baina yao. Ugomvi ulizidi hadi Morin akatoa bunduki na kumpiga risasi mdhulumiwa,” polisi wakasema.

Hata hivyo, mwanamume huyo hakujeruhiwa sana.

You can share this post!

Mswada kutua bungeni kutupa wafisadi ndani maisha

Ajipiga risasi akijaribu kuua kombamwiko

adminleo