• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:23 PM
AFYA: Faida za kunywa maziwa

AFYA: Faida za kunywa maziwa

Na MARGARET MAINA

[email protected]


MAZIWA hutupatia angalau vitamini zote kama vitamini A, D, E na K. Pia yana madini ya calcium.

Hujenga na kulainisha ngozi

Vitamini na virutubisho vilivyomo ndani ya maziwa ni muhimu kwa ajili ya ngozi bora.

Huimarisha meno

Maziwa ni chanzo bora cha madini ya kalisiamu yaani Calcium. Pia huzuia kutoboka na kuoza kwa meno. Kalisiamu hufyonzwa na miili yetu kukiwa na vitamini D.

Huimarisha mifupa

Watoto  wanahitaji kunywa maziwa ili kuimarisha ukuaji wao. Pia watu wazima wanahitaji kunywa maziwa ili kulinda na kuimarisha mifupa yao dhidi ya magonjwa kama vile udhaifu wa mifupa au kitaalamu Osteoporosis. Maradhi haya huzuiliwa kwa kalisiamu ipatikanayo kwenye maziwa na ambayo hufyonzwa kutokana na uwepo wa vitamini D.

Kujenga misuli

Maziwa yanachangia katika ukuaji wa misuli. Hili ni kutokana na protini zinazopatikana kwenye maziwa. Wanariadha wengi hunywa maziwa baada ya mazoezi. Hii ni kwa ajili ya kuupa mwili virutubisho vya kutosha kwa ajili ya kujijenga tena. Maziwa huzuia maumivu ya misuli pamoja na kurudisha ute ulipotea kwenye misuli wakati wa kazi mbalimbali.

Kupunguza uzani

Wanawake wanaokunywa maziwa hupunguza uzito zaidi kuliko wale wasiokunywa. Inashuriwa kunywa maziwa wakati wa chakula cha jioni au unapokula matunda. Pia maziwa yanaweza kutumiwa kama kileta hamu ya kula chakula (appetiser).

Huzuia maumivu wakati wa hedhi

Wanawake wengi hupata maumivu wakati wa hedhi. Maziwa yamethibitishwa kuzuia na kupunguza maumivu haya kwa kiasi kikubwa.

Huongeza nguvu mwilini

Je, unaishiwa nguvu mapema au kuchoka sana? Unahitaji virutubisho vilivyomo kwenye maziwa. Hivi vitaupa mwili wako nguvu mpya na kukufanya kuwa mwenye nguvu siku nzima.

Huondoa kiungulia

Kiungulia husababishwa na asidi zipatikanazo tumboni. Hivyo maziwa (ambayo si mgando) hutengeneza utando maalumu tumboni ambao hupambana na asidi hizi.

Kwa hiyo unywaji wa maziwa (ambayo si mgando) utakusaidia kupambana na tatizo la kiungulia.

Hupambana na maradhi mengine

Utafiti umebaini kuwa maziwa huzuia magonjwa. Magonjwa au hali hizi ni kama vile shinikizo la damu. Inaaminika pia maziwa hupunguza lehemu (cholesterol) mwilini na kuongeza uwezo wa macho kuona vizuri.

You can share this post!

NIPE NIKUPE: Manchester United mizanini ikiwazuru Wolves...

MAPISHI: Ugali na sukumawiki

adminleo