• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 6:55 PM
MAPISHI: Sambusa za mboga

MAPISHI: Sambusa za mboga

Na MARGARET MAINA

[email protected]

 

Kuandaa: Dakika 20

Muda wa kupika: Dakika 20

Walaji : 3

Sambusa katika hatua ya maandalizi. Picha/ Margaret Maina

Vinavyohitajika

  • Viazi ulaya 3 vilivyochemshwa kisha uvikate vipande vidogovidogo
  • Njegere (peas) zilichemshwa kidogo ½  kikombe
  • Vitunguu 2 kata vipande vidogo
  • Tangawizi ½
  • Pilipili 2
  • Bizari kijiko ½
  • Giligilani iliyosagwa kijiko 1
  • Garam masala nusu kijiko
  • Majani ya curry 4
  • Juisi ya limau kijiko 1
  • Mafuta kijiko 1 cha kupikia
  • Chumvi
  • Karoti 2; katakata
  • Unga wa ngano vijiko 4 au ute wa yai
  • Chapati dough

Maelekezo

  • Kwenye kinu, weka tangawizi, kitunguu saumu na pilipili. Twanga kwa pamoja hadi vilainike kisha hifadhi pembeni.
  • Bandika sufuria au kikaangio jikoni. Weka mafuta, yakipata moto weka, bizari na majani ya curry. Pika kwa dakika 2 huku ukigeuza mara kwa mara. Weka mchanganyiko wa pilipili kisha pika hadi harufu ya kitunguu saumu na tangawizi ipotee.
  • Weka kitunguu maji, pika kwa dakika mbili kisha weka mboga yoyote ya majani utakayopenda.
  • Weka viazi ulaya, unga wa giligilani, bizari, garam masala na chumvi.  Changanya vizuri mpaka viazi vichanganyikane na viungo vingine.
  • Punguza moto uwe wa wastani, pika kwa dakika tano huku ukikoroga taratibu. Weka njegere na limau. Changanya vizuri kisha pika kwa dakika mbili hivi. Toa motoni na acha mboga zipoe kabisa.
  • Koroga unga wa ngano au ute wa yai, hii itakusaidia kufungia sambusa.
  • Kata manda kwenye umbo la pembetatu kisha weka mboga mboga kiasi. Anza kufunga ila ukifika mwisho paka ute wa yai au unga wa ngano uliokoroga. Inasaidia sambusa zisifunguke wakati wa kupika.
  • Bandika kikaango chenye mafuta jikoni. Mafuta yakipata moto anza kupika sambusa hadi zigeuke rangi na kua kahawia. Yatoe na hifadhi pembeni. Rudia hii hatua hadi sambusa zote ziive.

Sambusa zikishapoa, pakua na ufurahie na wenzako.

You can share this post!

Mama wa Taifa aongoza usajili wa Huduma Namba Ikulu

MKU yafadhili ujenzi wa darasa nchini Rwanda

adminleo