• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 2:16 PM
Usain Bolt aahidi kufichua klabu ya soka aliyojiunga nayo

Usain Bolt aahidi kufichua klabu ya soka aliyojiunga nayo

Na GEOFFREY ANENE

MSHIKILIZI wa rekodi za dunia za mbio za mita 100 na mita 200, Usain Bolt amesema amepata klabu ya kusakatia soka yake ya malipo.

Mjamaica huyu mwenye umri wa miaka 31 aliyestaafu kutoka riadha mwaka 2017, ametangaza Jumatatu kwamba atafichua klabu hiyo Februari 27, 2018 (saa tano asubuhi saa ya Afrika Mashariki).

Tovuti ya Vanguard nchini Nigeria imemnukuu akisema, “Nimejiunga na klabu moja ya soka. Fahamu jina ya klabu hiyo Jumanne (8am GMT).”

Kwa mujibu wa tovuti hiyo, shabiki huyu sugu wa Manchester United aliratibiwa kufanyiwa majaribio na klabu ya Borussia Dortmund nchini Ujerumani mwezi ujao wa Machi.

Alifanya mazoezi na mabingwa wa zamani wa Afrika, Mamelodi Sundowns, kutoka Afrika Kusini mwezi Januari mwaka 2018.

“Mojawapo ya ndoto yangu kubwa ni kujiunga na Manchester United. Hata hivyo, Dortmund ikiridhika na mimi, nitajiunga nayo na kujitahidi vilivyo mazoezini.

Nimeongea na (kocha wa zamani wa United) Alex Ferguson na kumueleza anahitaji kuishawishi kwa maneno matamu. Aliniambia nikiwa fiti na tayari, atajaribu kadri ya uwezo wake kutimiza ndoto yangu,” amesema.

You can share this post!

Nakumatt yamumunywa kama pipi na Nkana ya Zambia

BI TAIFA FEBRUARI 27, 2018

adminleo