• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 12:47 PM
MAPISHI: Makaroni na nyama

MAPISHI: Makaroni na nyama

Na MARGARET MAINA

[email protected]

MUDA wa kuandaa: Dakika 25

Muda wa kupika: dakika 15

Walaji: 2

Vinanyohitajika

  • Makaroni nusu pakiti (pima kulingana na mahitaji yako)
  • Nyanya 4
  • Nyanya ya kopo (tomato paste) vijiko 3
  • Vitunguu maji 2
  • Kitunguu saumu 1
  • Pilipili mboga 1
  • Soy sauce kwa kijiko kidogo
  • Chumvi kijiko 1 kidogo
  • Giligilani kijiko 1 kikubwa
  • Gharam masala ¼ kijiko kidogo
  • Binzari kijiko 1 kidogo
  • Tangawizi ½ kijiko kidogo
  • Nazi 1 iliyokomaa
  • Njegere glasi 1
  • Biringani 1, kate vipande virefu na vyembamba
  • Italian seasoning kijiko 1 kidogo
  • Pilipili ndefu 2; kata vipande vidogovidogo
  • Cayenne pepper yaani udaha kijiko 1 kidogo

Maelekezo

  • Andaa viungo – menya nyanya, vitunguu maji viwili, pilipili mboga na kitunguu saumu. Kata vipande vidogo. Kamua tui la nazi.
  • Andaa njegere, zichemshe ila zisiive sana. Epua.
  • Kwenye sufuria, weka maji na chumvi, acha yachemke.
  • Weka makaroni, pika kwa dakika 10 kisha epua.  (fuata muda elekezi kwenye paketi ya makaroni)
  • Chuja maji, hifadhi.
  • Ni vizuri ukipika makaroni dakika moja au mbili chini ya muda elekezi kwenye paketi, hii itafanya makaroni yaive vizuri yakichanganywa na sauce na wakati wa kumalizia kupika.
  • Weka mafuta ya kupikia kwenye sufuria, bandika jikoni.
  • Acha mafuta yapate moto vizuri kisha weka kitunguu maji. Hakikisha moto ni mkali ili mboga ziive vizuri bila kuchuja maji.
  • Pika kwa dakika mbili huku unakoroga.
  • Weka kitunguu saumu, bizari, tangawizi, pilipili ndefu, giligilani ya unga, italian season na gharam masala.
  • Koroga vizuri kisha weka nyanya. Koroga taratibu kisha acha ziive hadi zitengane na mafuta. Weka nyanya ya kopo (tomato paste) na biringani na ukoroge pamoja.
  • Weka njegere, koroga pamoja. Weka soy sauce pamoja na chumvi kiasi.
  • Weka makaroni kwenye sufuria. Changanya na sauce ya nyanya na njegere. Weka pilipili mboga, koroga na acha ziive kiasi, ili harufu iwe tamu na nzuri. Weka tui la nazi.
  • Geuza mara kwa mara kisha acha chakula kichemke kidogo. Nyunyizia cayenne pepper na pilipili manga ichanganye na chakula kisha epua.

Chakula kikishakuwa tayari, pakua na ufurahie.

You can share this post!

ULIMBWENDE NA AFYA: Manufaa ya limau

Tabia za ushoga zaripotiwa Juja

adminleo