• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Apigwa na butwaa demu kutafuna nyama kilo moja

Apigwa na butwaa demu kutafuna nyama kilo moja

Na TOBBIE WEKESA

UGENYA, SIAYA

KALAMENI mmoja alipigwa na butwaa baada ya mrembo kutafuna kilo moja ya nyama peke yake.

Kulingana na mdokezi, ilikuwa ni siku yake ya kwanza kukutana na mrembo ana kwa ana. Wawili hao walikutana Facebook, wakajuana na kisha wakaanza harakati za kuchumbiana.

Inadaiwa polo alimuomba mrembo wakutane katika hoteli ili waweze kujuana zaidi. Mrembo alikubali ombi la polo la kukutana. Polo alianza kuwaza ni kitu gani angemnunulia ili afurahie.

Duru zinaarifu kwamba mrembo alipowasili, polo aliagiza kilo moja ya nyama choma, kuku robo na chupa kadhaa za soda. Penyenye zinasema baada ya weita kuandaa meza, mrembo aliivamia nyama kwa fujo. Polo aliamua kula kuku choma kwa vile hakuwa mraibu wa nyama choma.

Muda si muda, sahani ilibakia tupu. Polo alibaki kumtazama tu huku akitamani kucheka. “Kwani ulikuwa na njaa gani! Tangu uinamishe kichwa hutaki kutazama juu,” polo alimuuliza mrembo kwa mshangao. Mrembo alienda moja kwa moja hadi kwa soda na kuanza kuteremsha kana kwamba hakusikia maneno ya polo.

Polo aliendelea kula kuku wake bila haraka. Baada ya muda mfupi, mrembo alimaliza kunywa soda. “Nikuongezee nyama nyingine?” polo alimuuliza mrembo kwa utani.

Mrembo alimuangalia polo na kumshukuru. “Nashukuru sana kwa kuninunulia nyama. Mimi napenda sana kula nyama choma. Hata kesho tukikutana, ninunulie tu choma. Sitaki kitu kingine,” mrembo alimueleza polo.

Tukio hili lilimshangaza polo zaidi. “Unamaanisha umekula nyama kilo moja peke yako na kuimaliza? Na bado ukaongezea soda. Kwani tumbo lako ni pana aje?” polo alishangaa.

Inadaiwa mazungumzo aliyotaka polo na mrembo hayakufanyika tena.

“Najua umeshiba. Tutazungumza tutakapokutana tena,” polo aliamka akalipa chakula na kuondoka.

You can share this post!

Mchakato wa kumng’oa Jaji Maraga waanza

Kalameni afukuzwa kanisani kwa kulemewa kutoa sadaka na...

adminleo