• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 6:55 AM
Kalameni afukuzwa kanisani kwa kulemewa kutoa sadaka na fungu la kumi

Kalameni afukuzwa kanisani kwa kulemewa kutoa sadaka na fungu la kumi

Na LEAH MAKENA

MUTHAMBI, CHOGORIA

POLO wa hapa alijipata pabaya pale jina lake lilipoondolewa kwenye sajili ya washirika wa kanisa kwa madai kwamba alizembea kutoa sadaka.

Penyenye zasema kuwa pasta alianza kulalamika kuwa washiriki hawakuwa wakitoa sadaka wakidai hali ya maisha ilikuwa imewalemea.

Yasemekana pasta aliagiza uchunguzi ili kubaini waliokuwa wamechukua muda mrefu bila kutoa sadaka na fungu la kumi.

“Hili kanisa haliwezi kusonga mbele bila pesa. Kila siku mnapata kikombe cha chai baada ya ibada pamoja na huduma zingine za bure. Mnataka tuendeshe ibada vipi iwapo nyinyi sio waaminifu kwa kutoa sadaka?” pasta aliteta.

Baada ya kufanya kazi yao, wachunguzi walimkabidhi mchungaji orodha ya washiriki waliokuwa wamezembea kutoa fungu la kumi kwa muda wa miezi kumi mtawalia.

Kulingana na mdokezi, baada ya kukagua orodha, pasta alimkabidhi jamaa barua ya kumpiga marufuku kuwa mshiriki wa kanisa kwa kutotoa chochote kwa mwaka mmoja.

Minong’ono yasema kuwa baadhi ya washiriki walikashifu hatua ya pasta ila wakashindwa kumkosoa hadharani kwa kuogopa kutengwa.

You can share this post!

Apigwa na butwaa demu kutafuna nyama kilo moja

Mtoto aliyepotea apatikana amefariki ndani ya gari la askofu

adminleo