• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 10:10 AM
Ukosefu wa mvua kulemaza ukuaji wa uchumi

Ukosefu wa mvua kulemaza ukuaji wa uchumi

Na BERNARDINE MUTANU

Ukuaji wa uchumi nchini Kenya utatatizika kutokana na upungufu wa mvua nchini.

Ripoti hii ni kwa mujibu wa gavana wa Benki Kuu ya Kenya Patrick Njoroge ambaye alionya kuwa ukame utaathiri ukusanyaji wa ushuru na ukuaji wa nafasi mpya za kazi.

Dkt Njoroge alisema athari za ukame kwa kilimo itafanya ukuaji wa uchumi kwenda chini 2019 hadi asilimia 5.3 kutoka asilimia 6.3 zilizokadiriwa.

Utakuwa ukuaji wa pili wa chini zaidi katika uchumi tangu serikali ya Jubilee kuingia mamlakani 2013.

Dkt Njoroge alisema hayo wakati wa mahojiano na Bloomberg, “Kama kutakuwa na ukame, basi ukuaji wa uchumi utashuka hadi asilimia 5.3 au chini au zaidi kidogo ya kiwango hicho,” alisema.

Ukuaji wa chini wa uchumi utaathiri mapato ya makampuni, na kusababisha kiwango cha ushuru kinachokusanywa kwenda chini, hivyo kuathiri zaidi nafasi za kazi.

Alisema hali huenda ikawa ilivyokuwa 2017 ambapo ukuaji wa uchumi ulikuwa ni asilimia 4.9 kutoka asilimia 5.9 mwaka uliotangulia.

Hii uni kutokana na kupungua kwa kiwango cha mazao ya shambani kwa asilimia 1.6 mwaka wa 2017 kutoka asilimia 4.7 mwaka uliotangulia na asilimia 5.3 mwaka wa 2015.

Kilimo ndio uti wa mgongo wa Kenya na huchangia thuluthi moja ya ukuaji wa uchumi wa Kenya. Pia, uhimili robo tatu za bidhaa za Kenya zinazouzwa nje ya nchi.

You can share this post!

Euronuts wasema Sh1 milioni za Chapa Dimba ni zao

EABL yatangaza kuongeza bei ya pombe

adminleo