• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
UMBEA: Upendo hauna husuda na huwa hauhesabu mabaya

UMBEA: Upendo hauna husuda na huwa hauhesabu mabaya

Haya ni mazoea rahisi ambayo unaweza kujifunza na kuyafanyia kazi kila siku. Hata hivyo wengi wetu hatuna utaratibu wa kuuliza tunapohitaji kitu kwa wenzetu wala kusema asante pale tunapopata kile tukitakacho. Kwamba unaona kila jambo ni haki yako na hauna sababu ya kusema asante. Ni vyema kuwa na mazoea ya kusema asante, ni neno dogo ambalo lina nguvu kubwa.

Eleza hisia zako kwa mwenzako, mweleze kwamba unampenda na jambo ambalo linakuvutia kwake. Ni vizuri kueleza hisia zako kwa wale walioleta tofauti chanya katika maisha yako. Siku hizi kuna mazoea ya kutuma ujumbe mfupi ama kupiga simu kuzungumza na walio karibu ya maisha yetu. Ni vyema upate muda mara kwa mara wa kuzungumza nao ana kwa ana. Mazungumzo ya uso kwa uso yanaleta ukaribu zaidi ya kutumia njia za kisasa za mawasiliano. Inapobidi, onana na unayeongea naye.

Siku zote huwa na mtu anayehitaji jambo moja ama lingine. Unaposaidia watu wengine utajisikia vizuri katika nafsi yako. Yule unayemsaidia anaweza kuwa jirani yako, jamaa yako ama nduguyo ambaye alihitaji jambo ama kitu ambacho unao uwezo wa kumsaidia.
Unapojitolea kumsaidia mtu mwingine, usitarajie malipo kwa jinsi moja ama nyingine, kwani kama unatarajia malipo, bila shaka utakuwa hutendi hivyo kwa kujitolea.

  • Iwapo unakuwa na wakati mgumu kueleza hisia zako kwa mwenzako, mwandikie barua

Mueleze yale yaliyomo moyoni mwako kumhusu na umuwekee barua hiyo mahali ambako anaweza kuiona. Kwani wengine ni rahisi zaidi kuandika kuliko kuzungumza.

  • Katika yote jifunze kusamehe

Kama unapenda ama unampenda mtu utambue kwamba siku zote hawezi kuwa mtilimifu. Yapo mambo ambayo yatakukwaza, usiyaweke moyoni, mweleze inapobidi na uyaache yaende zake.

Upendo hauna husuda na huwa hauhesabu mabaya.

You can share this post!

MWANAMKE MWELEDI: Mkondo wa maisha yake ulibadilika ghafla

DAU LA MAISHA: Bidii yake yatambuliwa kazini

adminleo