• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 6:55 PM
#MashemejiDerby: Kivumbi Kasarani

#MashemejiDerby: Kivumbi Kasarani

Na GEOFFREY ANENE

Kivumbi kinatarajiwa katika mechi inayosubiriwa kwa hamu kubwa katika kalenda ya soka ya Kenya wakati mahasimu wa tangu jadi AFC Leaopards na Gor Mahia watashuka katika uwanja wa kimataifa wa Kasarani kwa mechi ya Ligi Kuu ya raundi ya 31, Jumamosi (4.15pm).

Mashabiki wa klabu zote pamoja na makocha wa timu hizi Andre Casa Mbungo (Leopards) na Hassan Oktay (Gor) wamesema timu zao ziko tayari kulambisha mwenzake sakafu.

Mashabiki walianza kumiminika katikati ya jiji la Nairobi mapema asubuhi wakiimba, kupiga ngoma na kucheza densi na kutaniana.

Wale wa Leopards wanasema leo Gor ‘lazima ilale’, huku wale wa Gor wakisema imezoa kupiga Leopards na hawatarijii kitu tofauti katika gozi hili lao la 91.

Mashabiki walitumia muda mwingi katika ya jiji la Nairobi kujipasha moto kabla ya mchuano huo wenye umuhimu mkubwa wa Gor kunyakua taji lake la 18 leo ama sherehe zao zicheleweshwe.

Pande zote zitateremka katika uwanja wa Kasarani unapbeba mashabiki 60, 000 zikiuguza vichapo baada ya Leopards kupepetwa 1-0 na KCB nayo Gor ikapokea dozi sawa na hiyo kutoka kwa Nzoia Sugar mnamo Mei 15.

Baadhi ya wachezaji wanaotarajiwa kutambisha katika gozi hili ni Whyvonne Isuza na Brian Marita kwa upande wa Leopards inayoshikilia nafasi ya 10 kwa alama 39 nayo Gor inajivunia wachezaji nyota kama Jacques Tuyisenge kutoka Rwanda na Francis Kahata.

Gor ikipata ushindi ama hata sare itatawazwa bingwa wa ligi hii ya klabu 18 ikiwa nambari mbili Bandari italemewa na nambari 16 Zoo mjini Mombasa, leo.

Vikosi vitarajiwa: AFC Leopards – Ezekiel Owade, Isaac Kipyegon, Dennis Sikhayi, Christopher Oruchum, Robinson Kamura, Said Tsuma, Eugene Mukangula, Musa Assad, Boniface Mukhekhe, Jaffari Owiti, Aziz Okaka, Jairus Adira, Soter Kayumba, David Ochieng’, Austin Odhiambo, Brian Marita, Vincent Oburu, Yeka Wayi.

Gor Mahia – Peter Odhiambo, Philemon Otieno, Joash Onyango, Harun Shakava, Wellington Ochieng’, Francis Kahata, Kenneth Muguna, Boniface Omondi, Nicholas Kipkirui, Samuel Onyango, Jacques Tuyisenge, Geoffrey Ochieng, Joachim Oluoch, Ernest Wendo, Hashim Sempala, Erisa Ssekisambu, Francis Mustafa, Boniface Oluoch.

You can share this post!

Makundi ya ‘Tangatanga’ na...

Mkewe Gideon Moi akataa kazi ya serikali

adminleo