• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Kalameni aliyezaa na dada apanga kumuoa

Kalameni aliyezaa na dada apanga kumuoa

Na BENSON MATHEKA

RUNDA, NAIROBI

KALAMENI mmoja mjini hapa amefichua kuwa alizaa na dada yake wa kambo na kwamba anampenda sana na ameapa kumuoa.

Jamaa huyo alisema aliamua kumwaga mtama kwa sababu ya mapenzi yake kwa mwanadada huyo ambaye tunafahamishwa ni mrembo ajabu.

Hata hivyo, jamaa alisema japo anampenda mwanadada huyo ana hakika wazazi wake hawatafurahi kufahamu kwamba wamekuwa wakifanya mapenzi hadi wakapata mtoto. “Dada yangu kwa kambo ana mtoto wangu. Tulianza kufanya mapenzi miaka mitatu iliyopita hadi akapata mimba.

Aliniahidi kwamba hakuna atakayejua vituko vyetu lakini sasa ninataka kumuoa kwa sababu ndiye mama ya mtoto wangu,” jamaa alimfichulia rafiki yake ambaye alishtuka.

Kulingana na jamaa huyo mwenye umri wa miaka 26, alianza kumtamani mwanadada huyo akiwa na umri wa miaka 17.

“Kilichoanza kama hisia za kawaida za mahaba miongoni mwa vijana kiligeuka na kuwa uhusiano thabiti wa mapenzi. Siwezi kumtoa katika moyo na mawazo yangu. Nampenda sana dada yangu wa kambo na lazima nitamuoa,” alisema jamaa ambaye ni meneja wa benki moja jijini Nairobi.

Kulingana na jamaa huyo, hataki mtoto wake kuishi bila baba na anajua kwamba ni mwiko kufanya mapenzi na kuoa mtu wa familia.

“Lakini kiwango ambacho uhusiano wangu na dada yangu wa kambo umefika ni tofauti. Kuna mtoto ambaye anakabiliwa na tisho la kuitwa mwanaharamu. Sitaki mtoto wangu aitwe mwanaharamu,” alisema.

Kwa vile anajua kwamba wameiletea aibu familia yake na yeye na dada yake wa kambo wameamua kuhama Kenya na tayari mwanadada huyo na mtoto wako ng’ambo. Jamaa anatarajiwa kuondoka Kenya mwishoni mwaka huu.

WAZO BONZO…

 

 

 

 

You can share this post!

Mwanamke aliyeshiriki ngono na mtoto aungama ana Ukimwi

Kidosho pabaya kupapasa polo mbele ya majirani

adminleo