• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 3:03 PM
Wanyama ashinda tuzo ya goli bora la Februari EPL

Wanyama ashinda tuzo ya goli bora la Februari EPL

Na GEOFFREY ANENE

VICTOR Wanyama ameshinda tuzo ya goli bora la mwezi wa Februari mwaka 2018 kwenye Ligi Kuu ya Uingereza, Ijumaa.

Nahodha huyu wa timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, aliwapiku mwanasoka bora wa Afrika mwaka 2017 Mohamed Salah (Liverpool & Misri) pamoja na Sergio Aguero (Manchester City & Argentina), Jose Izquierdo (Brighton & Hove Albion & Colombia), Adam Smith (Bournemouth & Uingereza) na Mario Lemina (Southampton & Gabon).

Kiungo huyu mkabaji wa Tottenham Hotspur alivuta kiki zito kutoka nje ya kisanduku lililosaidia klabu yake kutoka 2-2 dhidi ya Liverpool uwanjani Anfield hapo Februari 4.

Katika mchuano huo, Wanyama aliingia kama nguvu-mpya katika dakika ya 79 akijaza nafasi ya Mbelgiji Mousa Dembele. Aliona lango dakika moja baadaye akiisawazishia Spurs 1-1.

Mvamizi hodari Harry Kane alikosa nafasi ya kuweka Spurs 2-1 juu alipopoteza penalti dakika ya 87 kabla ya Salah kupachika bao tamu dakika ya 91 lililowania tuzo ya goli bora la Februari.

Kane alipata nafasi nyingine ya kufuma penalti dakika ya 95 na akaifunga, huku mechi hiyo ikatamatika 2-2. Salah alifunga mabao yote ya Liverpool dhidi ya Tottenham siku hiyo.

Bao la Aguero lilikuwa dhidi ya Leicester City mnamo Februari 10.

You can share this post!

Kirwa, Cheshari na Kosgei kushiriki Hannover Marathon

Kenya yang’aa kwenye tenisi U-12

adminleo