• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Maumivu ya tumbo hayapo tena, Kipsang’ ashinda Tokushima Marathon

Maumivu ya tumbo hayapo tena, Kipsang’ ashinda Tokushima Marathon

Na GEOFFREY ANENE

MKIMBIAJI shupavu Wilson Kipsang’ alinyakua taji la mbio za Tokushima Marathon nchini Japan mnamo Jumapili, mwezi mmoja baada ya kusalimu amri katika Tokyo Marathon.

Raia huyu wa Kenya, ambaye maumivu ya tumbo yalifanya ashindwe kutetea taji la Tokyo Marathon mnamo Februari 26, alitawazwa bingwa wa Tokushima kwa saa 2:19:35.

Muda huu ulikuwa nje ya rekodi ya Tokushima Marathon ya 2:15:25, ambayo Mjapani Yuki Kawauchi alitimka mwaka 2014

Bingwa huyu wa London Marathon mwaka 2012 na 2014 alifuatwa unyounyo na Mjapani Takumi Matsumoto katika mbio hizi zilizovutia wakimbiaji 12,400.

Mshikilizi huyu wa zamani wa rekodi ya dunia yuko katika harakati za kuanzisha hazina ya kusaidia kulinda mazingira na masomo ya watoto nchini Kenya kupitia mbio mbalimbali anazoshiriki.

Katika makala ya Tokyo Marathon mwaka 2018, Kipsang’ alikuwa ameahidi kuvunja rekodi ya dunia ya Mkenya mwenzake Dennis Kimetto ya saa 2:02:57 iliyowekwa mwaka 2014 jijini Berlin, Ujerumani. Hata hivyo, baada ya kilomita 15, aliumwa tumbo na kuamua kujizulu. Mkenya Dickson Chumba aliibuka bingwa kwa saa 2:05:30.

You can share this post!

Maafisa ndani kwa kumeza hela za makaburi

Mkali wa kriketi motoni kwa kubadilisha hali ya mpira kwa...

adminleo