• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Mamaye Wanyama abwagwa uchaguzini

Mamaye Wanyama abwagwa uchaguzini

Na GEOFFREY ANENE

MWENYEKITI wa Shirikisho la Mpira wa Pete (Netiboli) la Kenya (KNF) Mildred Ayiemba Wanyama Jumatatu amepoteza kiti hicho.

Mama huyu wa viungo Victor Mugubi (Tottenham Hotspur, Uingereza) na McDonald Mariga (Real Oviedo, Uhispania), aliambulia kura saba dhidi ya 54 za mshindi Immaculate Kabutha katika uchaguzi mkuu wa shirikisho hilo uliofanywa katika ukumbi wa City Hall jijini Nairobi mnamo Machi24, 2018.

Mbali na mama ya viungo hao wa Harambee Stars kupoteza nyadhifa zao, katibu wa muda mrefu wa KNF Lilian Anupi pia hakuwa na lake.

Anupi, ambaye amehudumu KNF kwa zaidi ya miaka 20, alibwagwa kwa kura 52-9 na Millicent Busolo.

Kiti cha Mwekahazina pia kimepata afisa mpya baada ya Anne Bett kulemea Sophie Makoba 53-7. Esther Mukene hakutetea kiti hiki chake.

Bett atasaidiwa na Evelyn Cherono aliyepata kura 43 dhidi ya wapinzani wake Eunice Okal (13) na Silphosa Omollo (tano).

Jonah Chemagut ni naibu wa rais. Hakuwa na mpinzani. Juma Amollo ni katibu msaidizi na John Makau (mpanga ratiba) na Suleiman Hassan (naibu mpanga ratiba).

You can share this post!

Ajenti wa M-Pesa kizimbani kuhusu njama ya kumtapeli Sabina...

GSU ya Kenya yapata kundi rahisi kwenye droo ya voliboli...

adminleo