• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 8:27 PM
Maafisa ndani kwa kumeza hela za makaburi

Maafisa ndani kwa kumeza hela za makaburi

Afisa wa usoroveya Cephas Kamande (kushoto) na afisa wa masuala ya ununuzi katika wizara ya serikali za mitaa Boniface Okerosi Misera waliofungwa kwa kuilaghai serikali pesa za makaburi. Picha/ Richard Munguti

Na RICHARD MUNGUTI

MAAFISA wawili wakuu katika kaunti ya Nairobi Ijumaa walihukumiwa kifungo cha miaka miwili kwa kuilaghai serikali zaidi ya Sh283 milioni katika kashfa ya ununuzi wa shamba la kuwazika wafu katika eneo la Athi River kaunti ya Machakos miaka tisa iliyopita.

Mbali na kifungo hicho cha miaka miwili kavu wawili hao waliagizwa walipe faini ya Sh77milioni.

Mahakama ilisema baraza la jiji la Nairobi NCC iliyokuwa inauziwa shamba hili ilipata liko na mawe na “makaburi hayangechimbika”

“Lilikuwa shamba la mawe. Hakuna mfu angelizikwa mle. Serikali ilipoteza mamilioni ya pesa kununua shamba la mawe. Maiti hutakiwa kuzikwa katika ardhi iliyo na mchanga mwingi,” alisema hakimu mwandamizi Feliz Kombo.

Wafungwa hao miwili ni  afisa wa usorovea Cephas Kamande na afisa wa masuala ya ununuzi katika wizara ya serikali za mitaa Boniface Okerosi Misera.

Akipitisha hukumu, Bw Kombo alisema maafisa hawa walikuwa wamepewa jukumu la kutunza pesa za umma lakini wakazifuja.

“Wawili hawa walikuwa wamepewa jukumu la kutunza pesa za umma lakini walizitumia vibaya waliponunua shamba lenye mawe la kuwazika wafu,” alisema Bw Kombo.

Wawili hao walikuwa wameshtakiwa pamoja na aliyekuwa Meya wa Nairobi Bw Geoffrey Majiwa, aliyekuwa naibu wa katibu mkuu wa lililokuwa baraza la jiji la Nairobi sasa kaunti ya Nairobi Bw Charo Kahindi.

Wengine wanaoshtakiwa kwa kupokea pesa katika kashfa na kutumia mamlaka ya afisi zao vibaya ni  pamoja na katibu wa zamani  Sammy Kirui, aliyekuwa katibu wa baraza la jiji la Nairobi Bw John Gakuo na katibu mkuu wa zamani Bw William Mayaka.

You can share this post!

Viongozi wa kidini: Weta na Mudavadi wakomeshe siasa za...

Maumivu ya tumbo hayapo tena, Kipsang’ ashinda...

adminleo