• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Wakenya sasa kufanya biashara popote Afrika bila vikwazo

Wakenya sasa kufanya biashara popote Afrika bila vikwazo

Na CECIL ODONGO

HATIMAYE Serikali imeidhinisha mkataba wa kibiashara ambao utawezesha Wakenya kufanya biashara katika mataifa mengine ya Afrika bila vikwazo vya usafiri.

Baraza la Mawaziri lilipitisha makubaliano ambayo Rais Uhuru Kenyatta alitia saini wiki jana kwenye mkutano wa Biashara Huru Barani Afrika, jijini Kigali, Rwanda.

Kwenye mpango huo, raia wa Afrika watasafiri kutumia paspoti moja. Pia sarafu moja ya barani itazinduliwa kurahisisha ununuzi na uuzaji.

Mswada ulioidhinishwa na mawaziri, sasa utapelekwa bungeni kujadiliwa na kupitishwa ili kuifanya Kenya kuwa mojawapo ya nchi 22 ambazo zimeanza kuitumia kama sheria.

Rais Uhuru Kenyatta aliongoza mkutano wa baraza hilo uliohudhuriwa pia na Naibu Rais William Ruto ambapo sekta ya kibinafsi ilitakiwa kutumia nafasi kutiwa saini kwa makubaliano hayo kuwekeza katika mataifa yote barani.

Makubaliano hayo ya Kigali yatawezesha bara la Afrika kupanua soko lake la kibiashara, kuimarisha miundo msingi na kuimarisha uchumi kwa zaidi za wananchi wake 1.2 bilioni.

Ikitekelezwa, vile vile itakuwa rahisi mno kutatua mizozo iliyokithiri sana miongoni mwa mataifa ya barani ikiwemo mizozo ya kila mara kuhusu mipaka na mapinduzi ya kijeshi.

Mkutano huo pia uliidhinisha uhuru wa kibiashara kwa Mashirika ya COMESA, SADC na EAC na bajeti la ziada kwa lengo la kupunguza gharama ya matumizi.

Baada ya kupitisha bajeti ya ziada, bajeti ya mwaka 2017-2018 pia itaangaliwa upya ili kupunguza nchi kukimbilia mikopo na kufanya nchi kushughulikia miradi yake kutokana na uwezo wake kiuchumi.

guzo nne za muhimu za awamu ya pili ya Rais Kenyatta pia zitatekelezwa kikamilifu ili kuimarisha uchumi wa nchi.

Baraza la Mawaziri pia lilijadili mswada wa kustaafu kwa maafisa wa kaunti na ripoti iliyotolewa majuzi kuhusu viwango vya umaskini nchini na Shirika la Takwimu Nchini(KNBS)

Mkutano huo ulipendekeza serikali itumie matokeo ya ripoti hiyo kutekeleza na kuipa kipaumbele miradi inayowainua wananchi kiuchumi ili kupunguza kiwango cha umaskini.

 

 

You can share this post!

France 24 yaungana na Signet kufaidi wenye runinga za...

Kila mwanahisa wa Eveready apokea Sh1 kwa kila hisa

adminleo