• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 12:48 PM
Girona ya Olunga yaharamisha uvutaji sigara

Girona ya Olunga yaharamisha uvutaji sigara

Na GEOFFREY ANENE

KLABU anayochezea Mkenya Michael Olunga, Girona FC, imeimarisha vita dhidi ya uvutaji wa sigara kwenye sehemu za mashabiki ya uwanja wake wa Montilivi.

Taarifa kutoka klabu hii inayoshiriki Ligi Kuu ya Uhispania zimesema Alhamisi kwamba Girona inataka wavutaji sigara wabadilishe sigara kwa tufaa.

Girona imeimarisha vita dhidi ya uvutaji wa sigara ndani ya uwanja wake kwa sababu inalenga kulinda mashabiki wasiovuta sigara wakiwemo walio na umri mdogo.

“Ni muhimu kuepuka kuvuta sigara katika sehemu ya mashabiki. Wahusika wanaombwa kukoma kuvutia sigara katika maeneo ya mashabiki. Ikiwa ni lazima wavute sigara, basi tutawatengea sehemu yao maalum, mbali na mashabiki ambao wanataka kufurahia mechi bila ya kukerwa na harufu ya sigara,” Girona imesema kwenye tovuti yake.

Girona imeongeza kwamba itaendeleza mikakati ya kuimarisha mazingira mazuri ya afya na yasiyo na bughudha kwa mashabiki.

“Huu ni mwanzo tu wa baadhi ya hatua tunapanga kuchukua kuhakikisha mashabiki wa umri zote wanafurahia soka pamoja na familia zao ndani ya uwanja wa Montilivi. Tumeanzisha kampeni ya kuhamasisha umma kuhusu hatua hii kupitia video.

“Katika mechi ijayo, kwa mfano, wavutaji sigara watashawisha kubadilisha sigara kwa kupewa tunda la tufaa. Klabu hii inapanga kuendeleza maadili ya afya, heshima na kulinda watu hasa watu walio na umri mdogo,” Girona imesema kwenye tovuti yake.

You can share this post!

Rwanda kutua nchini kwa mchuano wa Kombe la Afrika U-20

Mathare kuchupa juu ya Gor wakiilima Chemelil Sugar

adminleo