• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 12:48 PM
Gor yakanusha kutowalipa wachezaji licha ya kutatizika kifedha

Gor yakanusha kutowalipa wachezaji licha ya kutatizika kifedha

Na GEOFFREY ANENE

AFISA mmoja wa Gor Mahia amekiri kwamba mabingwa hao mara 16 wa Kenya wanakumbwa na matatizo ya kifedha.

Hata hivyo, Ronald Ngala, ambaye ni naibu wa katibu wa klabu hii, amepuulizia mbali ripoti kwamba Gor haijalipa wachezaji wake.

Amenukuliwa na tovuti ya klabu hiyo akisema, “Ni uongo mtupu (kwamba hatujalipa wachezaji). Tumewalipa na ripoti zinazoenea kwamba hatujalipa wachezaji wetu ni za kupotosha. Timu zote (nchini Kenya) zinapitia ugumu huu wa kifedha, si Gor Mahia pekee yake….”

“Tumewahi kuwa katika hali hii na tukafaulu kujikwamua kwa hivyo naamini tutafaulu tena,” aliongeza.

Gor Mahia, ambayo itapiga mechi yake ya saba ya Ligi Kuu itakapoalika Vihiga United mjini Kisumu hapo Jumapili, inashiriki mashindano ya Afrika ya Confederations Cup.

Itakuwa mwenyeji wa SuperSport United hapo Aprili 6 kabla ya kuelekea nchini Afrika Kusini kwa mechi ya marudiano mnamo Aprili 17.

You can share this post!

Jeraha lapona, Cherop sasa kushiriki mbio za Rome Marathon

LSK yakerwa na mazoea ya maafisa wa serikali kudharau sheria

adminleo