• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 5:55 AM
Joho amtembelea Miguna hospitalini Dubai

Joho amtembelea Miguna hospitalini Dubai

WINNIE ATIENO na CHARLES WASONGA

GAVANA wa Mombasa Ali Hassan Joho Alhamisi alimtembelea mwanaharakati wa NASA Dkt Miguna Miguna ambaye anapokea matibabu katika hospitali moja nchini Dubai. 

Msemaji wa Joho Richard Chacha alisema gavana huyo alimtembelea Dkt Miguna kumjulia hali na kumtia moyo.

“Mheshimiwa Joho yuko nchini Dubai. Atamtembelea Dkt Miguna ambaye amelazwa katika hospitali moja katika uwanja wa ndege wa Dubai. Tutawatumia picha na maelezo zaidi,” Bw Chacha akasema kwa njia ya simu.

Gavana Joho amekuwa katika ziara rasmi ya wiki moja katika eneo la Estonia, Dubai.

You can share this post!

Ni kama drama! Miguna akumbana na masaibu zaidi wakati wa...

‘Ni kibarua kigumu kumsaidia Miguna’

adminleo